Somalia : Fyekelea mbali balozi wa UN
SERIKALI ya Somalia imemwamuru Balozi wa Umoja wa Mataifa (UN) nchini hapa, Nicholas Haysom kuondoka kwa tuhuma za kuingilia masuala ya ndani ya taifa hili.MOGADISHU, SOMALIA Taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje imesema Haysom hakaribishwi tena Somalia na hawezi kuendelea kuendesha shughuli zake. Hatua hiyo imetokea baada ya balozi huyo kuandika barua akiihoji Serikali maswali mengi kuhusu hatua zilizochukuliwa wakati wa makabiliano yaliyotokea katika mji wa Baidoa, Jimbo la Kusini Magharibi. Makabiliano hayo yalihusiana na kukamatwa kwa naibu kiongozi wa zamani wa wanamgambo wa al-Shabaab, Sheikh Mukhtar Robow Abu Mansur mwezi uliopita. Haysom alikosoa kukamatwa na kuuawa kwa waandamanaji waliokuwa wakipinga kukamatwa kwa Roobow kati ya Desemba 13 na 15, mwaka jana. Balozi huyo alikuwa amemwandikia barua Waziri wa Mambo ya Ndani, Mohamed Abukar Islow na kuzungumzia uzito wa taarifa ambazo zilikuwa zimewahusisha wanajeshi wanaoungwa mkono na UN na
Comments