Posts

Showing posts from January 13, 2019

BIOLOGY FORM ONE

CHEMISTRY FORM ONE

ACADEMIC BOOKS

Image
               <<<  OPEN HERE  BIOLOGY FORM TWO BIOLOGY FORM THREE   BIOLOGY FORM FOUR     <<OPEN HERE>>   <OPEN HERE>>                                        <<PHYSICS FORM FOUR>> <<PHYSICS FORM THREE>> <<PHYSICS FORM TWO >> <<PHYSICS FORM ONE>> PHYSICS SYLLABUS O- LEVEL     PHYSICS SYLLABUS A-LEVEL  BIOLOGY SYLLABUS O-LEVEL    BIOLOGY SYLLABUS A- LEVEL CHEMISTRY SYLLABUS O-LEVEL CHEMISTRY SYLLABUS A-LEVEL GEOGRAPHY SYLLABUS O-LEVEL GEOGRAPHY SYLLABUS A-LEVEL

CHEMISTRY FORM THREE

HABARI ZA LEO JUMAPILI 13/1/2019

Image

Waziri awaonya madaktari nchini

Image
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amewaonya madaktari kote nchini kuacha tabia za kuwa madalali wa Maduka ya dawa kwa kuwaandikia wagonjwa dawa mara mbili mbili. Waziri Ummy ameagiza hospitali za Rufaa kote nchini kuhakikisha zinakuwa na maduka ya dawa litakalokuwa  na uhakika wa dawa zote muhimu ili kuondosha kero hiyo na kuondoa mianya ya madaktari kudalalia dawa kwenye maduka binafsi. Hata hivyo amesema kuwa watakaobainika watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Waumini wamgeuka Imam msikitini, wataka aongoze maandamano

Image
Imam mwenye ushawishi mkubwa jijini Khartoum nchini Sudan amezongwa na waumini akiwa msikitini wakimtaka awaongoze kufanya maandamano dhidi ya Serikali ya Rais Omar al-Bashir. Video iliyosambazwa kwenye mitandao ya kijamii inawaonesha baadhi ya waumini wakipaza sauti mbele ya Imam huyo, “amka utuongoze kuandamana kutoka hapa msikitini.” Umati wa watu walitoka msikitini wakipiga kelele za kutaka Serikali iliyopo madarakani iachie ngazi. Polisi waliofika katika eneo hilo walifyatua mabomu ya machozi kuwatawanya waandamanaji waliojikusanya baada ya ibada ya Ijumaa. Katika kipindi cha wiki mbili za maandamano ya kupinga Serikali, watu 22 wameripotiwa kupoteza maisha. Okwi, Kagere walivyowapasua JS Saoura 3-0 Kwa mujibu wa Reuters, maandamano yaliyoshuhudiwa jana ni makubwa kuliko yaliyokuwa yamefanyika awali. DC Njombe awapa neno Wajasiliamali Maandamano yalianza Desemba 19 mwaka huu baada ya Serikali kutangaza kupanda kwa bei za vyakula na mafuta, hali inayoda

Mpinzani apinga matokeo ya Urais wa DRC Mahakamani

Image
Aliyekuwa Mgombea wa Urais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) kwa tiketi ya chama cha upinzani, Martin Fayulu amefungua kesi katika Mahakama ya Kikatiba akipinga matokeo ya uchaguzi wa nchi hiyo. Tume ya Huru ya Uchaguzi ya Taifa (CENI), ilimtangaza mgombea mwingine wa upinzani Felix Tshisekedi kuwa mshindi wa uchaguzi huo uliofanyika Desemba 30 mwaka jana. Kwa mujibu wa takwimu za CENI, Tshisekedi alipata kura milioni 7 huku Fayulu akipata kura milioni 6.4 na mgombea wa chama tawala mmanuel Shadary akiambulia kura Milioni 4.4. Feli Ekombe ambaye ni mwanasheria wa Fayulu amesema kuwa katika kesi hiyo, mteja wake anataka Mahakama ifute matokeo yaliyotangazwa na CENI yanayombua Tshisekedi kama Rais mteule wa taifa hilo la Afrika ya Kati. Marekani, Ufaransa na Uingereza vimetaka kutoa ufafanuzi wa kina wa namna matokeo hayo yalivyopatikana. Wiki iliyopita, Kanisa Katoliki lenye ushawishi mkubwa nchini humo, kupitia kwa Baraza la Maaskofu lilieleza kuwa matokeo yaliyotanga

Makumi wapoteza maisha kwenye mlipuko wa tenki la mafuta

Image
on Makumi wapoteza maisha kwenye mlipuko wa tenki la mafuta Watu kumi na wawili wamepoteza maisha nchini Nigeria baada ya tenki la mafuta kulipuka mwishoni mwa wiki, kwa mujibu wa taarifa ya polisi. Tukio hilo limesababisha vifo vya watu kutokana na mlipuko wa matenki ya mafuta nchini humo kufikia mamia ndani ya kipindi cha miaka ya hivi karibuni, kutokana na watu kutoboa matenki hayo kwa lengo la kukusanya mafuta. “Tumekusanya miili 12 ya watu waliopoteza maisha pamoja na watu 22 waliojeruhiwa vibaya kutokana na kuungua na tumewapeleka hospitalini,” msemaji wa Polisi, Irene Ugbo ameiambia Associated Press jana. Amesema kuwa mlipuko huo ulitokea Ijumaa jioni katika eneo la Odukpani kwenye jimbo la Cross River. Baadhi ya mashuhuda waliohojiwa wamedai kuwa idadi kuwa idadi ya waliopoteza maisha wanafikia 60 na kwamba miili mingine haikuchukuliwa na polisi.

Video: Mnyika amvaa Spika Ndugai, Maajabu 8 ya Zanzibar

Image
Mnyika amvaa Spika Ndugai, Maajabu 8 ya Zanzibar, Ubunge 2020 mwiba kwa wateule wa JPM, Muswada vyama vya siasa bado moto, Shein ahimiza uzalendo kulinda Muungano, Wapinzani wamjibu Rais Magufuli…,Bofya hapa kutazama habari zilizopewa kipaumbele katika kurasa za mbele za magazeti ya leo Januari 13, 2019.

NEEMA!: Wazee 25499 kutibiwa bure wilayani Magu

Image
Halmashauri ya wilaya ya Magu mkoani Mwanza imefanikiwa kuwakabidhi wazee 25499 vitambulisho kwa ajili ya kupata matibabu bure. Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya hiyo, Dkt. Philemon Sengati wakati akikabidhi vitambulisho hivyo kwa wazee hao, ambapo amesema kuwa serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Magufuli imejipanga kuhakikisha wazee wote nchini wanapata matibabu bila malipo kama walivyoahidiwa mwaka 2015 wakati wa kampeni. Amesema kuwa mbali na kuwakabidhi vitambulisho wazee hao, pia limetengwa dirisha maalum kwa ajili ya utoaji wa huduma kwa wazee ili kurahisisha kufikia huduma bila kupanga foleni kutokana na umri wao. Naye mkurugenzi mtendaji wa halmashauri hiyo, Lutengano Mwaliba ameipongeza Idara ya Ustawi wa Jamii kwa utekelezaji wa ahadi ya serikali kwa kuwapatia wazee vitambulisho vya huduma za kiafya na kuwataka wazee wote waliotimiza miaka 60 kufika ofisini kwake ili waweze kuandikishwa na kupatiwa vitambulisho kwa ajili ya matibabu. Kwa upande wao wazee wameiponge