Posts

Showing posts from December 26, 2018

Tabora:Wauguzi wanaotoa lugha chafu waonywa

Image
WAUGUZI na watoa huduma za afya wa zahanati, vituo vya afya na hospitali mkoani Tabora, wametakiwa kufuata maadili ya kazi yao na kuacha kutoa lugha chafu zenye maudhi au kebehi kwa akinamama wajawazito wanaoenda kupata huduma. Onyo hiyo, limetolewa juzi na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Mkoa wa Tabora, Mwajuma Mhina ambaye alisema baadhi ya akinamama wakiwemo wajawazito wamekuwa wakitendewa ukatili na wauguzi kwa kutolewa lugha chafu afya jambo ambalo ni kinyume na maadili ya kazi hiyo. Alisema wauguzi kama hao hawawezi kufumbiwa macho kwa kuwa vitendo vya vinadhalilisha utu wa mwanamke na kuwaomba kutoa huduma kwa kuzingatia maadili na misingi ya kazi. “Huu ni unyanyasaji kwa akinamama, unawezaje kutoa lugha zisizofaa wakati wa mgonjwa akihitaji umuhudumie, umesomea kuwahudumia huo ndiyo wajibu wako utimize.., lakini kwa kuwa wapo wasiosikia tunaiomba Serikali kupitia wizara ya afya kufuatilia na kuwachukuliwa hatua,”alisema. Al

Z’bar: Naibu waziri atoa mazito kwa wanafunzi

Image
Na Khamis Sharif-ZANAIBAR NAIBU Waziri wa  Wizara  ya Kazi, Uwezeshaji,  Wazee ,Wanawake na Watoto, Shadya Mohamed Suleiman amewataka wanafunzi wa Jimbo la Magomeni kushughulikia masomo yao na kujiepusha na mambo ya tamaa kwani  yanaweza kuwapelekea kutofikia malengo yao. Hayo aliyasema hivi karibuni alipokuwa akizungumza katika utaoji wa zawadi katika shule za Jimbo la Magomeni wakati wa sherehe ya utoaji wa zawadi kwa wanafunzi waliofaulu kuingia michepuo , kidato cha pili na kidato cha tano kwa mwaka 2017/2018. Alisema ili wafanikiwe zaidi katika elimu ni lazima wawe wasikivu na wavumilivu kwa kufuata ushauri wa walimu ndipo watafanikiwa kwani elimu ndio mustakabali mzima wa maisha  na kuwataka waongeze bidii katika masomo  kwani wao ndio wataalamu  watarajiwa wa hapo baadae. “Acheni tamaa za kutamani vitu ambavyo wazazi hawana uwezo navyo mambo haya ndio yanayoweza kukuharibieni malengo yenu mliojiwekea ya baadae shuhulikieni masomo yenu,” a

CCM Morogoro watoa sifa hizi

Image
i Na MWANDISHI WETU-DAR ES SALAAM CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), Mkoa wa Morogoro kimewataka wananchi wote kumpa moyo Rais Dk. John Magufuli, kwani kazi anayoifanya chini ya serikali yake ni ya kishujaa kwa Watanzania wote. Pamoja na hali hiyo chama hicho kimewataka wananchi kuzidisha bidii ya kazi na uzalishaji wenye tija kwa manufaa pindi wanapokuwa kwenye ofisi zao, viwandani au mashambani. Akizungumza na waandishi wa habari jana mjini hapa, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Morogoro, Innocent Kalogeresi alisema wananchi, viongozi , wanaharakati  na wanasiasa , wote  wana wajibu wa kutokuwa wepesi kurubuniwa au kununuliwa utu wao kwa kushiriki  usaliti. “Rais Magufuli ni shujaa wa kweli wa maendeleo katika Taifa letu na kwa hali hii Watanzania wote kwa umoja na mshikamano wetu tumpe ushirikiano wa kila aina. “Tanzania ni moja na itabaki moja daima kwani  ni miongoni mwa nchi yenye hazina kubwa katika nchi za Kusini mwa Afrika iliohifadhi wapigania uhuru,” alisema Ka

Kampuni ya Setewico yalia

Image
Na MWANDISHI WETU-DODOMA UTITIRI wa kodi ambazo zinalipwa na wawekezaji nchini bado umeonekana kuwa changamoto kubwa kwao na hivyo kutoa ombi kwa Serikali ya Awamu ya Tano chini ya Rais Dk. John Magufuli kuangalia namna ya kupunguza utitiri huo wa kodi hizo. Ombi hilo limetolewa hivi karibuni jijini hapa na Mkurugenzi wa Ushirikiano na Uhusiano wa Jamii wa Kampuni ya Cetewico Limited,  Katrin Boehl alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari waliofanya ziara katika kiwanda hicho. “Kwa upande wangu lazima niseme nimeona ushirikiano wa hali ya juu  katika Serikali yangu Dodoma kwani nikiwa na tatizo lolote ninakwenda katika ofisi za Serikali yangu ya Dodoma, hivyo imeonesha uthamini  wa kiwango kikubwa wa  kazi tunazofanya,” alisema Katrin. Alisema kampuni yao inapongeza juhudi za Serikali katika ujenzi wa Tanzania ya viwanda nchini ili kufikia uchumi wa kati na wamedhamiria kuunga mkono kwa vitendo kauli mbiu ya Hapa Kazi Tu lakini changamoto kubwa amb

BoT yataja faida za dhamana za serikal

Image
Na MWANDISHI WETU-DAR ES SALAAM WATANZANIA wameshauriwa kushiriki kikamilifu katika minada ya dhamana za Serikali kwani faida zake ni kubwa kwa Taifa ikiwamo kufanya shughuli za maendeleo kwa kutumia fedha zake za ndani. Hayo yamesemwa hivi karibuni mjini Dodoma na Mkurugenzi wa Masoko na Fedha wa Benki Kuu ya Tanzania(BoT),  Alexander Ng’winamila wakati akiwasilisha mada katika mafunzo kwa waandishi wa habari za uchumi na fedha yalioandaliwa na BoT kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kuandika habari za fedha na uchumi. Akizungumza wakati akitoa mada inayohusu uwekezaji katika dhamana za Serikali; faida zake kwa Taifa na wawekezaji ambapo pamoja na mambo mengine amezungumzia umuhimu wa wananchi kushiriki kikamilifu kwenye midana ya dhamana za Serikali. Alisema bado kuna haja kwa vyombo vya habari kuendelea kutoa elimu kwa wananchi ili waweze kujua na kushiriki kikamilifu  katika minada hiyo. “Ombi letu kwa vyombo vya habari tunaomba muendelee kuelimisha umma kuhusu umuhimu wa

jifunze kufaham ugonjwa Wa Chango La Uzazi - (Mke/Mume)

Image
Tunapozungumzia mgonjwa wa chango tuna maana kuwa ni matatizo yaliyopo katika viungo vya uzazi kwa mke au mume. Huu ni ugonjwa ambao humpata mtu katika umri mdogo utotoni. Kwa mfano :- mume, hupata maumivu ya tumbo mara kueneza anapokuwa mdogo. Kwa upande wa mwanamke hupata maumivu ya tumbo anapoanza kuvunja ungo. Maumivu hayo hupelekea mtu (mume/mwanamke) kupata madhara katika viungo vyake vya uzazi. DALILI ZAKE Kwa mwanaume atakuwa akishiriki tendo la ndoa, anawahi sana kufika kileleni na kurudia mara nyingine ni vigumu sana. Pia mwanaume hatakuwa na uwezo wa kusimamisha. Ni vigumu kumpa mimba mwanamke Mwanamke mwenye chango la uzazi ana dalili zifuatazo:- Kupata maumivu makali wakati anapokaribia kuingia katika siku zake za hedhi Kuhisi maumivu makali wakati wa kushiriki tendo la ndoa Siku zake za hedhi hazitakuwa na ratiba, zitakuwa zinabadilika badilika Hujisikia homa kali anapokaribia siku zake za dhedhi Kupatwa hasirakali/ jazba anapokaribia kuingia kat

Askari polisi amchoma mwanafunzi kwa pasi ya umeme

Image
Tukio hili limetokea  tarehe 20/12/2018 majira ya 19:30hrs ambapo Jeshi la Polisi lilipata taarifa kuwa huko maeneo ya Mtaa wa Lumaliza kata ya Mbugani Manispaa ya Tabora  kijana mmoja aitwaye  JUMANNE NTIMIZI, HUSSEIN, Miaka 17, Mwanafunzi kidato cha tatu katika shule ya sekondari Cheyo, alijeruhiwa na Askari  anayefahamika kwa jina la E.9301 CPL ALMAS   kwa kuchomwa  na pasi ya umeme sehemu mbalimbali za mwili wake na kisha kupigwa na kitu kizito kwenye paji la uso, mdomoni na kumsababishia maumivu makali mwilini. Chanzo cha tukio hili ni kutokana na  kijana JUMANNE NTIMIZI kukutwa  na bwana ALMAS  akiwa amemkumbatia binti yake aitwaye AMINA ALMASI, Miaka 17, Mwanafunzi wa kidato cha tatu shule ya sekondari Cheyo karibu na nyumba yake  kwa nia ya kufanya mapenzi ndipo baba mzazi wa Binti huyo alipochukua hatua ya kufanya kitendo hicho kibaya. Akiongea na waandishi wa habari Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora    ACP – EMMANUEL NLEY amesema  Jeshi la Polisi mkoa wa

MAGAZETI YA LEO 26/12/2018

Image