Posts

Showing posts from December 22, 2018

Tsunami Indonesia:Watu zaidi ya 40 wafariki dunia na 600 kujeruhiwa

Image
Watu zaidi ya 40 wamefariki dunia na wengine zaidi ya 600 kujeruhiwa kufuatia mawimbi ya tsunami yenye ukubwa wa mita 20 katika Mlango Bahari wa Sunda, ambayo yameharibu pia majumba kadhaa zikiwemo hoteli za kitalii. Eneo lililoathirika vibaya kwa tsunami hii ni mkoa wa Pandeglang katika jimbo la Banten kwenye kisiwa cha Java, ambacho kina hifadhi ya taifa ya Ujung Kulon na fukwe maarufu, kwa mujibu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Majanga. Katika waliopoteza maisha, 33 wanatokea mkoa huo. Katika mji wa Bandar Lampung kusini mwa kisiwa cha Sumatra, mamia ya wakaazi walihifadhiwa kwenye jengo la ofisi moja ya serikali. Mkaazi mmoja wa wilaya ya Pandeglang aliyejitambulisha kwa jina la Alif alisema wimbi la tsunami kwenye eneo lao lilifikia ukubwa wa mita tatu. Alikiambia kituo cha televisheni cha MetroTV kwamba watu wengi walikuwa bado wanawatafuta jamaa zao waliopotea. "Nililazimika kukimbia wakati wimbi kubwa lilipokiuka ufukwe na kufika umbali wa mita tak

Watu 11 wa familia moja wanusurika kufa kisa kunywa togwa

Image
Picha ya mtandao Watu 11 wa familia moja wa kijiji cha Mtwarapachani, Namtumbo mkoani Ruvuma, wamenusurika kifo baada ya kunywa pombe aina ya togwa. Wanafamilia hao kwa sasa wamelazwa katika Kituo cha Afya cha Namtumbo kwa  matibabu, Waliolazwa ni Tatu Ndumbaro (48), Maisha Ndumbaro (14), Issa Ndumbaro (5), Mariamu Issa Ndumbaro (48), Daima Ndumbaro (29) na Khadija Ndumbaro (12). Wengine ni Asha Omari (80), Asheri Uega (31), Safiruna Omari (32), Matokeo Ndumbaro (13) na Bahati Ndumbaro(25) ambao wote ni wa familia moja ya Ndumbaro walioko katika kijiji hicho. Mganga Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo, Dk. Yuna Hamisi, alikiri kuwapo kwa wagonjwa hao katika kituo hicho cha afya na kwamba timu ya madaktari ikiongozwa na Godwin Luta iko kituoni hapo kuhakikisha wanaokoa maisha yao. Mganga aliyeshiriki katika uchunguzi huo, Dk. Luta, alisema baada ya kuwachunguza wagonjwa hao walibaini ugonjwa huo wa kutapika na kuharisha ulisababishwa na kitu walichokula katika fami

MAGAZETI YA LEO 23/12/2018

Image

Zifaham faida zitokanazo na limau kiafya

Image
Faida za limau au ndimu zinajumuisha matumizi kama tiba kwa ajili ya vidonda vya kooni, matatizo katika mmeng’enyo wa chakula, matatizo ya meno, homa, kuvuja damu ndani ya mwili, baridi yabisi, kutibu malengelenge, uzito kupita kiasi, matatizo katika mfumo wa upumuwaji, kipindupindu na shinikizo la juu la damu. Pia ni dawa nzuri kwa ajili ya nywele na ngozi. Tangu karne nyingi limau linajulikana kama dawa, husaidia pia kuongeza kinga ya mwili, kusafisha tumbo na hujulikana pia kwa kazi yake nzuri ya kusafisha damu. Juisi ya limau ina faida kadhaa nyingi kama vile kuondoa mchanga katika figo, kupunguza kukamaa kwa mishipa (strokes) na kupunguza joto la mwili. Kama kinywaji ambacho huondoa uchovu mwilini, juisi ya limau itakusaidia kubaki mtulivu na mpole. Faida nyingi za limau zinatokana na virutubishi vyake vingi mhimu kwa mwili kama vile vitamini C, vitamini B6, vitamini A, vitamini E, folate, niacin thiamin, riboflavin, pantothenic acid, shaba, kalsiamu, chu

Mfanyabiashara Akram aachiwa kwa kulipa faini ya sh milioni 259

Image
Na Kulwa Mzee-DAR ES SALAAM MFANYABIASHARA Akram Azizi aliyekuwa akikabiliwa na mashtaka 75 ya uhujumu uchumi ikiwamo ya kukutwa na nyara za Serikali, silaha 70, risasi 6,496 na kutakatisha Dola 9,018 za Marekani,  amefutiwa mashtaka baada ya kulipa faini ya Sh milioni 259. Akramu alifutiwa mashtaka hayo jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kufunguliwa upya mashtaka 73 yakiwamo ya kukutwa na silaha bila kibali, kukutwa na risasi na kilo tano za nyama ya nyati. Mashtaka mapya yalisomwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri na Wakili wa Serikali Mkuu, Paul Kadushi, akisaidiana na Wakili Simon Wankyo. Katika mashtaka 75 yaliyofutwa anadaiwa kuyatenda makosa hayo kati ya Juni na Oktoba 30 na 31, mwaka huu katika maeneo ya Oysterbay. Katika shtaka la kwanza anadaiwa Oktoba 30, mwaka huu maeneo ya Oysterbay alikutwa na meno sita ya tembo yenye thamani ya Sh 103,095,000. Shtaka la pili anadaiwa Oktoba 30, mwaka huu alikutwa na kilo 65 ya nyama

IMTU yazalisha madaktari 1,478

Image
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam CHUO cha Kimataifa cha Sayansi ya Tiba na Teknolojia (IMTU), kimefanikiwa kuzalisha madaktari 1,478 na watumishi 2,279 wa sekta ya afya wanaofanya kazi katika maeneo mbalimbali nchini na wengine nje ya nchi. Kauli hiyo ilitolewa Dar es Salaam mwishoni mwa wiki na Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu, Marten Lumbanga, wakati wa mahafali ya 11 ya chuo hicho kwa wahitimu wa shahada ya udaktari na stashahada ya uuguzi. Lumbanga ambaye ni mjumbe wa bodi ya chuo hicho, alisema ni habari njema kusikia kuwa zaidi ya nusu ya waganga wakuu wa wilaya (DMO) katika maeneo mbalimbali nchini walihitimu IMTU. “Hii ni habari njema inayotutia moyo hasa kwenu nyinyi wahitimu kwa sababu naamini mtu kupewa nafasi ya DMO lazima aonyeshe uwezo mkubwa wa kitaaluma, uwajibikaji na uhusiano mzuri baina yake na watumishi walio chini yake, wagonjwa na jamii kwa jumla,” alisema. Kuhusu tishio la Tume ya Vyuo Vikuu (TCU) kufuta usajili wa chuo h

Mbowe, Matiko kula krismasi mahabusu

Image
Krismasi mahabusu NA PATRICIA KIMELEMETA MWENYEKITI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe na Mbunge wa Tarime Mjini, Ester Matiko, watasherehekea Sikukuu ya Krismasi na mwaka mpya gerezani baada ya kufutiwa dhamana zao katika kesi ya uchochezi inayowakabili viongozi hao na wengine saba wa chama hicho. Baada ya kuahirishwa kwa kesi hiyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam jana, viongozi hao wawili waliwatakia wanachama wao heri ya Krismasi na mwaka mpya. Katika kesi hiyo, Wakili wa Serikali, Wankyo Simon, alidai mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Wilbard Mashauri, kuwa kesi imekuja kwa ajili ya kutajwa na kuiomba mahakama hiyo kupanga tarehe nyingine kwa madai kuwa hawana taarifa ya kinachoendelea mahakama ya juu. Hata hivyo, Wakili wa utetezi wa kesi hiyo, Faraja Mangula, alidai kuwa mawakili, Peter Kibatala na Sheck Mfinanga, wamepata dharura na kushindwa kufika mahakamani hapo na waliomba mahakama hiyo kuah

Mwanafunzi wa chuo afariki juu ya nguzo ya umeme

Image
Mwanafunzi mmoja wa chuo cha mafunzo Wilaya ya Wete, Pemba aliyejulikana kwa jina la, Hemed Suleima Seif (40) amefariki baada ya kupigwa na shoti ya umeme wakati akijaribu kufanya matengenezo. Fundi wa umeme Inaelezwa kuwa kabla ya kukutwa na umauti, mwanafunzi huyo alikuwa akifundishwa ujuzi wa matengenezo ya Umeme kwa vitendo na mwalimu wake. Akithibisha kutokea kwa tukio hilo, Kamanda wa polisi mkoa wa Kaskazini Pemba, Sheikhan Mohammed Sheikhan amesema tukio hilo limetokea saa 1:45 za asubuhi, wakati marehemu akiwa chini ya mwalimu wa fani hiyo wakijaribu kurekebisha kasoro katika moja ya nguzo ya jengo. “ Ni kweli tumepokea taarifa kutoka kwa wenzetu wa chuo cha mafunzo kuwa kuna mwanafunzi anaetambuliwa kwa jina la Hemed Suleiman, amefariki baada ya kupigwa na shoti ya umeme ,” amesema. “ Tayari

DIAMOND AFUNGUKA BAADA YA KUOMBA RADHI BASATA, WASAFI FESTIVAL INAENDELEA

Image
Msanii wa Bongo Fleva Nasibu Addul ‘Diamond’, alipokuwa akizungumza na Wanahabari (hawapo pichani), jana Nairobi Kenya. BAADA ya kufungiwa na Baraza La Sanaa Tanzania (BASATA), msanii Diamond pamoja na Rayvanny Desemba 21 mwaka huu, na baadaye kuomba radhi katika Baraza la Sanaa la taifa ‘BASATA’, tayari Diamond amelazimika kueleza makubaliano yake na baraza hilo jambo linalomfanya sasa aweze kuendelea na  tamasha lake la Wasafi Festival 2018 nchini Kenya. Akiwa nchini Kenya kwenye kikao chake  na waandishi wa habari alisema, “S erikali yetu inatupa sapoti kubwa sanahivyo  kilichotokea ni makosa yetu wenyewe kwani  wimbo wimbo wetu wa Mwanza  ni wazi ulikuwa  hautakiwi kufanyiwa shoo nchini kwentu, lakini kwa sisi wasanii kama mjuavyo tunapoikua jukwaani kuna muda huwa tunakuwa na  mizuka  ya kupitiliza nadhani ndicho kilichotokea kwetu kiasi cha kukosea na kujikuta Serikali yetu inatuadhibu kwa kufata za Baraza letu. “ Sisi tkuiwa kama moja wa raia wema nchini

Mapya Yaibuka, Aliyedaiwa Kufia Mwananyamala na Dawa za Kulevya Tumboni

Image
KAMISHNA Mkuu Wa Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Rogers Siyanga, amesema uchunguzi waliyoufanyika wamebaini kuwa mwili wa mfanyabiashara, Happy Mboya (38) aliyefariki dunia katika Hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam haukuwa na dawa za kulevya kama ilivyoripotiwa awali. Happy aliyefariki dunia Jumapili iliyopita Desemba 16, 2018 na mwili wake kupangwa kusafirishwa jana kwenda Moshi kwa mazishi, Polisi wa Kituo cha Oysterbay waliuchukua kwa ajili kuupeleka katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kwa ajili ya uchunguzi zaidi baada ya kudaiwa kuwa ulikuwa na madawa ya kulevya tumboni. Siyanga amesema maofisa wa Mamlaka hiyo walikuwepo wakati mwili wa marehemu Happy ukifanyiwa upasuaji na haukukutwa na dawa za kulevya kama ilivyodaiwa. Jana Siyanga alisema baada ya uchunguzi huo angetoa taarifa kamili juu ya tukio hilo. Baba mdogo wa marehemu, Ally Bilali jana alisema baada ya kurejea nchini, Happy alifikia katika nyumba ya kulala wageni ambayo haik

Kwa Simba Hii, Nkana wajipange upya

Image
WAKATI keshokutwa Jumapili, wakitarajiwa kucheza mechi ya marudiano dhidi ya Nkana FC ya Zambia, Kocha Mkuu wa Simba, Patrick Aussems, ametamba kwamba wanajua umuhimu wa mechi hiyo, hivyo wamejipanga kuhakikisha wanashinda. Kocha huyo raia wa Ubelg­iji amejinadi kuwa wanataka kuutumia vizuri uwanja wa nyumbani kushinda lakini lengo kubwa ni kutinga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika. Simba wana kibarua cha kupambana na Nkana ya Zambia kwenye mchezo wa marudiano baada ya ule wa awali nchini Zambia kupoteza kwa mabao 2-1, hiyo imemfanya kocha huyo kuelekeza mbinu zake zote katika kutimiza lengo la mchezo wa marudio. Mbelgiji huyo ameliambia Championi Ijumaa, kwamba amekiandaa kikosi chake na kuwaeleza juu ya umuhimu wa mechi hiyo ambayo imebeba tiketi yao ya kutinga hatua ya makundi lakini ameomba mashabiki waende kuwapa sapoti ya kutosha jambo ambalo litawatoa wapinzani mchezoni. “Tunafahamu hii ni mechi kubwa na muhimu kwetu, tayari tumejianda

Atolewa Hospitali Nchini Ujerumani

Image
Staa wa Bongo Fleva, Omary Nyembo. MUNGU mkubwa! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya staa wa Bongo Fleva, Omary Nyembo kutolewa katika hospitali ya University Hospital of Dusseldorf ya nchini Ujerumani alikokuwa amelazwa baada ya kupata nafuu na kupelekwa Mombasa nchini Kenya. Akizungumza na Risasi Jumamosi, baba mzazi wa staa huyo, Faraji Nyembo alisema anamshukuru Mungu na Watanzania kwa maombi yao kwani mwanaye huyo kwa sasa ana nafuu na amepelekwa Kenya kwa ajili ya kuhudhuria kliniki. Aliendelea kueleza kuwa kwa sasa afya ya Dimpoz imeendelea kuimarika ambapo amefanikiwa kuruhusiwa kutoka hospitali ikiwa ni baada ya kufanyiwa oparesheni kubwa ya koo na sasa yupo nchini Kenya anakofanya kliniki pamoja na kupumzika pia. “Mwanangu sasa anaendelea vizuri kwani upasuaji aliofanyiwa umempa nafuu na hivi ninavyoongea na wewe ameruhusiwa kutoka hospitali nchini Ujerumani na yupo Kenya anakofanyia kliniki yake akisimamiwa na meya wa Mombasa ambaye ndiye anayempatia m

Marehemu ahukumiwa kwa uhujumu uchumi

Image
ALIYEKUWA Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (Tarura), Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma ambaye kwa sasa ni marehemu, Mhandisi Godfrey Majuto, amehukumiwa kulipa faini ya Sh milioni 3.6 na Mahakama ya Wilaya ya Mpanda baada ya kutiwa hatiani kwa makosa ya uhujumu uchumi. Majuto alifikwa na umauti Desemba 4, mwaka huu wakati akiwa tayari ameshatoa utetezi wake mahakamani hapo. Hukumu hiyo ilitolewa mahakamani hapo jana na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda, Gasper Luoga, baada ya kuridhika na ushahidi uliotolewa mahakani hapo na upande wa mashitaka ulioita mashahidi 10. Mbali na Majuto, washitakiwa wengine katika kesi hiyo walikuwa ni Naomi Nko ambaye wakati huo alikuwa ni Kaimu   Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda, Peter Mwanoni, Beatus Bisesa, mkandarasi na Chiyando Matoke. Ilidaiwa mahakamani hapo na  Mwanasheria wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) Mkoa wa Katavi, Bahati Haule, kuwa  washitakiwa hao

FastJet yaanza kurudisha nauli za abiria

Image
Hatua hiyo imefikiwa baada ya Desemba 17, mwaka huu Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kuliagiza shirika hilo kuwarudishia fedha abiria wote walio kata tiketi au kuwatafutia nafasi za safari katika mashirika mengine. Msemaji wa shirika hilo, Lucy Mbogoro, amesema baadhi ya wateja wao walianza kurudishiwa fedha hizo Jumatatu wiki hii hasa kwa wateja walionunua tiketi kwa njia ya mtandao. “Jumatatu tulitoa tangazo kuwa tutaanza kushughulikia malipo ya wateja wetu pamoja na wadau wengine tunaofanya nao biashara, siku hiyo hiyo tulianza kushughulikia kwa wale walionunua kwa M-Pesa, Airtel Money na Tigo Pesa. “Ila kwa wale walionunua kwa ‘cash’ tulitangaza tutaanza kushughulikia malipo yao tarehe 20 na tayari tumeanza kulishughulikia hilo , tumekuwa tukiendelea na taratibu za benki kwa sababu hatuwezi kukaa na fedha nyingi, lazima tuzipeleke benk” amesema Lucy. Amesema katika urejeshaji wa fedha hizo, watatoa kipaumbele kwa wateja waliotarajia kusafiri kuanz

Afariki baada ya kujirusha kutoka ghorofa ya tatu

Image
Jengo la Rock City Mall Mwanaume mmoja aitwaye Musa Ally mwenye umri wa miaka 25, ambaye ni mkazi wa  mtaa wa Kiloleli wilayani Ilemela jijini Mwanza, amefariki dunia baada ya kujirusha kutoka gorofa ya 3 hadi chini katika jengo la Rocky City Mall. Kaimu kamanda wa polisi Mkoa wa Mwanza, Advera Bulimba amethibitisha kutokea kwa tukio hilo leo Desemba 21, majira ya saa 7:00 mchana. Kamanda amesema kuwa kijana huyo alikuwa amekuwa akilewa kupitiliza na ambapo Desemba 16, 2018 alikamatwa na kuwekwa kituo cha polisi Kirumba, kutokana na kulewa hadi kilevi kilipopungua ndipo akaachiwa huru. “Baada ya uchunguzi tumebaini kuwa kijana huyo amekuwa akilewa na kuwaambia watu kuwa yeye ni masikini na hana ajira hivyo asilaumiwe mtu yeyote kwakuwa hana wazazi hivyo uamzi huo amechukua yeye mwenyewe'', amesema Bulimba. Kamanda pia amesema kuwa wamekuta ujumbe ndani ya mfuko wa marehemu ambao unaeleza kuwa ana Shahada Sayansi ya kompyuta aliyoipata Chuo Kikuu c

Nafasi za ajira leo Dec 22

Image
Bonyeza Links zifuatazo Kusoma zaidi na Kuapply: 5 New Jobs at The University of Dar es Salaam 2 New Job Opportunities at Restless Development Tanzania Job Opportunity at Catholic Relief Services(CRS), Country Manager Jobs at International Residual Mechanism for Criminal Tribunals (IRMCT), Intern (Legal Affairs) Job Opportunity at Tanbreed Poultry Ltd (Interchick), HR Officer Job Opportunity at International Rescue Committee Tanzania, IT Assistant Job Opportunity at International Rescue Committee Tanzania, Stores Assistant Job Opportunity at International Rescue Committee (IRC), Warehouse Officer Nafasi zingine ingia  www.ajirayako.co.tz