Uchaguzi DRC: Kanisa Katoliki lasema kuna mshindi wa wazi uchaguzi wa urais
Serikali ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), imekemea ushawishi unaotolewa na kanisa Katoliki unaodai kuwa wanajua kiongozi aliyeshinda katika uchaguzi wa rais. Barnabe Kikaya Bin Karubi ambaye ni msemaji wa 'Common front for the Congo', ameiambia BBC kuwa "Jambo linalofanywa na kanisa ni kitu ambacho hakikubaliki, ni sawa na kuwaandaa watu kufanya mapinduzi". Serikali ya mseto imesisitiza kwamba ni Tume ya uchaguzi peke yake ndio inaweza kutangaza matokeo ya uchaguzi. Matokeo ya uchaguzi wa urais DRC 'kuchelewa' Huduma ya intaneti yafungwa DR Congo siku moja baada ya uchaguzi Wagombea wa upinzani walalamikia dosari uchaguzi DRC Kanisa Katoliki, ambalo lina ushawishi mkubwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, limesema kuwa kuna mshindi wazi wa urais katika uchaguzi uliofanyika Jumapili, kwa mujibu wa matokeo ambao wamefanikiwa kuyaona. Maaskofu wa kanisa hilo wamewataka watawala nchini humo kuwa wakweli na kutangaza matokeo hayo karib...
Comments