Posts

Showing posts from January 1, 2019

Songea kukopesha Wanawake na Vijana kukwama

on Songea yakwama kukopesha Wanawake na Vijan Manispaa ya songea mkoani Ruvuma, imeshindwa kuendelea kukopesha vikundi vya wanawake na vijana kupitia mapatoyake ya ndani, baada ya vikundi hivyo kushindwa kurejesha fedha za mikopo kwa wakati na vinadaiwa zaidi ya sh. milioni 59. Mkurugenzi wa manispaa hiyo, Tina Sekambo ametoa taarifa katika kikao cha kamati ya ushauri na maendeleo ya mkoa wa Ruvuma (RCC), kuwa vikundi vilivyoshindwa kurejesha mikopo vingi vilikopeshwa katika kipindi cha mwaka 2017/18, na hadi kufika mwezi novemba 2018, na nikikundi kimoja pekee ambacho kimeweza kupunguza deni lake. Katika kipindi hicho cha miaka miwili manispaa hiyo imeweza kuwakopesha wanawake na vijana fedha kupitia makusanyo yeke ya ndani asilimia 10 kila mwezi, ambapo sh. milioni 31.10 zimekopeshwa kwa vikundi vya wanawake, na vijana sh. milioni 28.1. kwa lengo la kupambana na umasikini kwa njia ya ujasiriamali kwa kufanya kazi za mikono, ikiwemo kilimo na biashara ndogo ndogo ili waweze k

Habari kubwa katika magazeti ya Tanzania leo Januari 2, 2019

Image
on Habari kubwa katika magazeti ya Tanzania leo Januari 2, 2019 Fahamu yote yaliyojiri katika Magazeti ya Tanzania leo Januari 2, 2019. Hapa unapata habari zote zilizopewa uzito katika kurasa za mbele na kurasa za nyuma za habari za michezo na burudani.                

Waziri Mkuu atoa ombi kwa Wananchi

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amewataka Wananchi kuendelea kushirikiana katika kuibua na kubuni miradi mbalimbali kwa ajili ya kuboresha maendeleo . Waziri Mkuu ameyasema hayo     wakati akipokea msaada wa vyumba viwili vya madarasa vikiwa na  madawati vyenye thamani ya sh. milioni 80 kutoka kwa bank ya CRDB, Kata ya Nachingwea Mkoani Lind i. “Nawaomba wananchi wenzangu tuendelee kushirikiana katika kuibua na kubuni miradi mbalimbali kwa ajili ya kuboresha maendeleo kwenye kata yetu ya Nachingwea.” alisema Majaliwa  Pia Waziri Mkuu alikabidhi kompyuta 20 kwa shule za sekondari tano ambazo ni Kassim Majaliwa, Likunja, Mnacho, Hawa Mchopa na Ruangwa.