Posts

Showing posts from January 8, 2019

MAGAZETI YA LEO 9/1/2019

Image
Fahamu yote yaliyojiri katika Magazeti ya Tanzania leo Januari 9, 2019. Hapa unapata habari zote zilizopewa uzito katika kurasa za mbele na kurasa za nyuma za habari za michezo na burudani  

MABURUNGUTU YA PESA MWANZA UTATA WAIBUKA!

Image
Mkuu wa Utawala wa Polisi Mkoa wa Mwanza, ACP Advera Bulimba M WANZA:  Tukio la Jeshi la Polisi jijini Mwanza kukamata kilo 323.6 za dhahabu na maburungutu ya fedha taslim kiasi cha shilingi milioni mia tatu na milioni tano (305,000,000), Jumamosi iliyopita, limeibua sintofahamu na utata mkubwa uliotawaliwa na maswali, Uwazi limedokezwa.   Taarifa za awali zilidai kuwa dhahabu na mamilioni hayo ya shilingi yalikuwa yakisafirishwa kuelekea mkoani Geita. Katika tukio hilo ambalo watuhumiwa watatu wanashikiliwa na jeshi hilo, dhahabu ilikamatwa ndani ya gari katika Kivuko cha Kigongo huku mamilioni hayo yakinaswa ndani ya gari kwenye Kivuko cha Kamanga jijini Mwanza. Kufuatia matukio hayo mawili, kuliibuka maswali mengi yenye utata na kwamba itakuwa ni miongoni mwa kesi zitakazovuta hisia za wengi kutokana na kiasi hicho kikubwa cha dhahabu na pesa zilizonaswa. “Mimi ninachojua ni kwamba mtu ukitaka kusafirisha kiasi kikubwa cha fedha lazima uombe ulinzi wa polisi. “S

MAJAMBAZI:! Alhaj Mzee Yusuph na Mkewe wavamiwa

Image
Aliyekuwa Msanii wa Taarabu nchini Alhaj Mzee Yusuph amevamiwa na Majambazi Usiku wa kuamkia Leo akiwa nyumbani kwake na familia yake. Kwa mujibu wa Mzee Yusuph ameeleza kuwa akiwa nyumbani kwake Chanika usiku huu na familia yake ghafla walivamiwa na majambazi watatu na walivyoingia mzee anasema alipiga makelele sana kuomba msaada kwa majirani lakini hakupata msaada. Pia amesema badala yake ikabidi apambane nao mwenyewe akitumia mawe na panga na kwasababu wavamizi hao hawakuwa na silaha za moto bali walitumia baruti kuwatisha watu wasisogee eneo la tukio hata hivyo walikimbia Ila walifanikiwa kuchukua simu na vitu vingine vidogovidogo, na Mke wake Leyla Rashidi amepata majeraha kidogo na hivyo amekimbizwa hospitali kwa ajili ya kupata matibabu

BREAKING NEWS: Waziri Angela Kairuki ahamishwa Wizara ya Madini

Image
Leo December 08, 2018 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli amefanya mabadiliko madogo kwenye baraza la mwaziri. Tatika mabadiliko hayo Angela Kairuki amehamishwa kutoka wizara ya madini na kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji, Doto Biteko akiwa Waziri Kamili wa wizara ya Madini.

Waziri Mkuu aibana kampuni inayodaiwa bil 2.9

Image
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameziagiza kampuni zote zinazosambaza nguzo za umeme kulipa ushuru wa halmashauri wanakotoa nguzo hizo amboa ni asilimia tano ya gharama ya kila nguzo kama ilivyoelekezwa na Sheria ya Fedha za Serikali za Mitaa. Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa Ametoa agizo hilo jana Jumatatu, Januari 7, 2019 baada ya kupata taarifa kuhusu kampuni ya New Forest ambayo inamkataba na TANESCO wa kusambaza nguzo za umeme, kukaidi kulipa ushuru wa asilimia tano ya gharama ya kila nguzo. Ushuru huo umefikia sh. bilioni 2.9 hali iliyopelekea uongozi wa mkoa kuzuia nguzo hizo zisitoke. Wiki iliyopita akiwa katika ziara ya mkoa Ruvuma, Waziri Mkuu alipokea malalamiko kuhusu mkoa wa Iringa kuzuia kusambazwa kwa nguzo za umeme ndipo alipoamua kuwaita Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Ally Happi pamoja na wakuu wa wilaya, wakurugenzi pamoja na wenyeviti wa halmashauri wanaotoka katika wilaya zinazozalisha nguzo. Viongozi wengine waliohudhuria kikao hicho ni