Posts

Showing posts from January 3, 2019

VIDEO: Ridhiwani Kikwete atoa ujumbe mkubwa na mzito kwa vijana

Image
Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete ametoa ujumbe mzito kwa vijana ambao wenye malengo ya kutaka kufanikiwa kimaisha. Ridhiwani amesema hayo wakati wa uzinduzi wa radio ya Hakuna Matata uliofanyika Alhamisi hii nya January 3, 2019 katika ukumbi wa Makumbusho ya Taifa iliyopo Posta jijini Dar es Salaam. TAZAMA FULL VIDEO HAPA CHINI.

Matukio 12 ya kukumbukwa duniani 2018

Image
MARKUS MPANGALA MWAKA 2018 unafika tamati kesho. Yapo matukio kadhaa ambayo yamevigusa vyombo mbalimbali duniani. Miongoni mwa matukio hayo yapo ya kiuchumi, kisiasa na kijamii pia kuna ya kusikitisha yaliyosababisha hata vifo. Haya ni baadhi ya matukio ya kukumbukwa katika mwaka huu 2018 ni:- Uzunduzi wa treni yenye kasi zaidi Afrika Taifa la Morocco lilizindua treni inayokwenda kwa kasi zaidi barani Afrika ambayo  imepunguza nusu ya muda wa kilometa 200 unaotumika kusafiri katika miji ya kibiashara na kiviwanda ya Casablanca na Tangier katika safari ya saa mbili. Uzinduzi huo ulifanywa na Mfalme Mohammed VI na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron.Treni hiyo inakwenda kwa kasi ya kilometa 320. Afrika inatazamia kuimarisha miundombinu ya usafiri kushinikiza biashara, uwiano na utangamano wa kieneo. Mataifa ya Afrika yanakumbatia mfumo wa reli ya mwendo kasi katika kujaribu kushinikiza na kukuza uchumi na kuimarisha kasi za kusafirisha bidhaa baina ya mataifa kibiashara.

Somalia : Fyekelea mbali balozi wa UN

Image
SERIKALI ya Somalia imemwamuru Balozi wa Umoja wa Mataifa (UN) nchini hapa, Nicholas Haysom kuondoka kwa tuhuma za kuingilia masuala ya ndani ya taifa hili.MOGADISHU, SOMALIA Taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje imesema Haysom hakaribishwi tena Somalia na hawezi kuendelea kuendesha shughuli zake. Hatua hiyo imetokea baada ya balozi huyo kuandika barua akiihoji Serikali maswali mengi kuhusu hatua zilizochukuliwa wakati wa makabiliano yaliyotokea katika mji wa Baidoa, Jimbo la Kusini Magharibi. Makabiliano hayo yalihusiana na kukamatwa kwa naibu kiongozi wa zamani wa wanamgambo wa al-Shabaab, Sheikh Mukhtar Robow Abu Mansur mwezi uliopita. Haysom alikosoa kukamatwa na kuuawa kwa waandamanaji waliokuwa wakipinga kukamatwa kwa Roobow kati ya Desemba 13 na 15, mwaka jana. Balozi huyo alikuwa amemwandikia barua Waziri wa Mambo ya Ndani, Mohamed Abukar Islow na kuzungumzia uzito wa taarifa ambazo zilikuwa zimewahusisha wanajeshi wanaoungwa mkono na UN na

Mdee:viongozi bora CCM 2018

Image
on Listi ya Mdee viongozi bora CCM 2018 Mbunge wa Kawe kupitia kiti cha Chadema ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake (BAWACHA), Halima Mdee kuelekea kuufunga mwaka 2018 na kuukaribisha mwaka 2019 amezungumzia viongozi wachache wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) chini ya Rais John Pombe Magufuli waliofanya vizuri katika kuwatumikia wananchi kwa mwaka 2018 katika serikali ya awamu ya tano. Kwenye orodha hiyo amewataja; Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Selemani Jafo, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William  Vangimembe  Lukuvi  na  Katibu Mkuu (TAMISEMI), Eng. Mussa Iyombe. ”Kidunchu sana naweza nikamtaja Katibu Mkuu wa Tamisemi, Iyombe yeye alijaribu kutuliza ‘temperature’ sababu alitoa ‘statement’ ambayo ni ya adimu sana kuisikia katika awamu hii”, Mdee. ”Jafo naye kidogo katika mawaziri wote ameonesha utofauti wa kuzungumza kile ambacho wengi wameogopa kuzungumza”, Mdee. ”Lukuvi naye kidogo ameonesha jitihada k

Habari kubwa katika magazeti ya Tanzania leo Januari 4, 2019

Image
Fahamu yote yaliyojiri katika Magazeti ya Tanzania leo Januari 4, 2019. Hapa unapata habari zote zilizopewa uzito katika kurasa za mbele na kurasa za nyuma za habari za michezo na burudani.

Mfahamishe na mfundishe mwanafunzi wako njia rahisi za kufaulu mtihani wake

Image
YAWEZEKANA ! Unasoma sana lakini matokeo yakitoka hutamani rafiki au hata wazazi wako wajue kile ulichopata AU unafanya vizuri darasani na mitihani ya kawaida lakini inapofika muda wa kufanya mitihani ya mwisho kama vile ya wilaya,mkoa na taifa unafeli mpaka unahisi unafanyiwa hila au umelogwa!. Kufeli sio jambo zuri kwa mtu kulipata katika kitu chochote hasa ukiwa shuleni,kwa kutambua hilo haijalishi wewe ni mwanafunzi wa shule ya hadhi gani au unarudia mtihani au wewe ni P.C huna budi kujua njia hizi rahisi sana za kukusaidia kufaulu mitihani yako. 1 . SOMA MITIHANI ILIYOPITA. (past papers) Njia hii ni rahisi sana itakusaidia sana kujua namna ya kujibu maswali,kujua mitego na mbinu za watunga mitihani ambao mara nyingi hurudia maswali yaleyale kwa namna tofauti, vilevile itakusaidia kujua format au miundo ya mitihani na hii itapelekea wewe kujua majibu ya maswali mengi sana ndani ya muda mfupi sana.Mbinu hii itakusaidia sana kufaulu mitihani. 2. JUA MADA ZOTE ZA

Bulaya amtaka Jenista ajiuzulu uwaziri

Image
WAZIRI Kivuli, Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu, Esther Bulaya amemtaka Waziri Jenista Mhagama ajali misingi ya uwajibikaji kwa kujiuzulu wadhifa wake kutokana na kushindwa kusimamia masilahi ya wafanyakazi. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, Bulaya ambaye ni Mbunge wa Bunda (Chadema), alisema hatua ya Rais  Dk. John Magufuli kutengua uteuzi wa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii (SSRA), Irene Isaka na kuwaacha wengine wanaotakiwa kuwajibika imeibua utata, kwa kuwa mkurugenzi huyo ni mtendaji tu. Alisema sheria ya mafao ya mwaka 2018 imempa Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu mamlaka ya moja kwa moja ya kutunga na kusimamia kanuni za ukokotoaji wa mafao, hivyo Jenista anatakiwa kuwajibika au laa awajibishwe kwa kutojali maoni ya wadau wakati wa utafutaji na upitishaji wa kikokotoo ambacho Rais Magufuli alikitengua. “Kutengua uteuzi wa Mkurugenzi wa SSRA na kum

Habari kubwa katika magazeti ya Tanzania leo Januari 3, 2019

Image
Fahamu yote yaliyojiri katika Magazeti ya Tanzania leo Januari 3, 2019. Hapa unapata habari zote zilizopewa uzito katika kurasa za mbele na kurasa za nyuma za habari za michezo na burudani.