Posts

Showing posts from December 25, 2018

Maajabu! :Mwanafunzi mdogo alawiti watoto wenzake,polisi wamtafuta

Image
Mwanafunzi wa darasa la tatu katika Shule ya Msingi ya Wilunze mwenye umri wa miaka 14 anatuhumiwa kuwalawiti wanafunzi wenzake ambapo katika tukio la hivi karibuni alimlawiti mtoto wa miaka mitatu. Hayo yalibainishwa na Mtendaji wa Kijiji Cha Wilunze Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma, Georgina Richard wakati akizungumza juzi katika mafunzo ya kuwajengea uwezo watendaji wa vijiji na kata kupitia mradi wa kutokomeza ukatili wa kijinsia, mimba na ndoa za utotoni unaotekelezwa na Shirika lisilokuwa la Kiserikali la Woman Wake Up (WOWAP). Alieleza kuwa tukio la kulawitiwa mtoto wa kiume wa miaka mitatu lilitokea Novemba 26, mwaka huu kijijini hapo. Alisema mtuhumiwa huyo ni mtoro wa kudumu na mara ya mwisho alikuwa akisoma darasa la tatu Shule ya Msingi Wilunze. Alisema siku ya tukio mtuhumiwa huyo alimuingiza mtoto huyo kwenye nyumba ambayo haijamalizika na kumfanyia kitendo hicho. “Aliyeshuhudia kitendo hicho ndio alikwenda kutoa taarifa kwa mama wa mtoto ambapo

Mawakala 10 wa Shirika la Ndege Tanzania Kizimbani kuhujumu uchumi

Image
Mawakala 10 wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, wakikabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi ikiwamo kulisababishia Shirika hasara, kujipatia fedha kwa njia ya udanganyifu na kutakatisha Sh. milioni 10.8. Washtakiwa hao walisomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Ally Salum. Wakili wa Serikali, Wankyo Simon, aliwataja washtakiwa hao kuwa ni, Fabian Ishengoma (34), Adam Kamara (27), Marlon Masubo (29), Neema Kisunda (24), Alexander Malongo (29) na Tunu Kiluvia (32). Wengine ni Jobu Mkumbwa (30), Mohammed Issah (38), Godfrey Mgomela, Absalom Ambilikile na Janeth Lubega. Upande wa Jamhuri ulidai kuwa kati ya Machi 10 na Oktoba 9, mwaka huu, mahali tofauti jijini Dar es Salaam na Mwanza washtakiwa kwa pamoja wakiwa mawakala wa ATCL, walilisababishia Shirika hilo hasara ya Sh.10,874,280. Katika shtaka la pili, ilidaiwa kuwa tarehe na mahali pa shtaka la kwanza, washtakiwa wote kwa pamoja walijipatia fedha

Takukuru mwanza yashinda kesi

Image
Na Paschal D.Lucas,Mwanza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Mwanza, imeshinda kesi Na. 15/2018 dhidi ya Maafisa Elimu wawili Bw. MUGUSI RICHARD ISANGA- Afisa Elimu Jiji la Mwanza na Bw. JAPHET MWIKABE BUCHA wa Manispaa ya Ilemela. Mnamo tarehe 06/02/2018 washitakiwa  walifikishwa Mahakamani kwa kosa  la kuomba na kupokea Rushwa ya sh 1,000,000/= kutoka kwa  Mwananchi  ili waweze kumsaidia mtoto wake kupata nafasi ya shule ya Bweni, ambapo ni kinyume na kifungu cha 15 (1) cha Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Na. 11/2007. Mnamo tarehe 14.12.2018, hukumu ya kesi hiyo ilitolewa na Hakimu Mkazi Mfawidhi Mheshimiwa  RODA NDIMILANGA ambapo  washitakiwa walikutwa na hatia na Mahakama ikawaamuru adhabu ya faini ya shilingi laki tatu (Tsh. 300,000/=) au kifungo cha miaka mitatu (3) jela kwa kila mmoja.

Msaidizi wa waziri ashikiliwa kwa tuhuma za kubaka

Image
Kwa kipindi cha wiki moja Jumla  ya makosa matano ya udhalilishaji yameripotiwa katika vituo mbali mbali ndani ya mkoa wa mjini magharib unguja. Akithibitisha kutokea kwa matukio hayo kwa waandishi wa Habari  Kamanda wa Jeshi La Polisi mkoa wa Mjini Unguja Thobias Sedoyeka alisema katika Matukio hayo watuhumiwa watatu wamekamatwa akiwemo Shabani Ali Othman miaka 32 Mkaazi wa Mpendae ambaye ni msaidizi binfsi wa waziri. Alisema Shaban anadaiwa kutenda kosa hilo Novemba 18 mwaka huu saa 10:00 jioni katika ofisi ya serikali, Maruhubi. Alisema mtuhumiwa anadaiwa kumpa kinywaji mshichana (jina linahifadhiwa) ambae pia ni mfanyakazi mwenzake na kusababisha kupoteza fahamu na hatimae kumbaka. Alisema uchunguzi bado unaendelea huku taratibu za kumfikisha mahakani mshitakiwa zikiendelea. Pia alisema jumla ya matukio matatu ya vifo yameripotiwa ambayo yalitokea baina ya Disemba 17 na 21 katika maeneo tofauti ya mkoa huo. Alisema Disemba 17 saa 10:00 jioni katika pwan

Bunge lavunjwa kuitisha uchaguzi mpya 2019

Image
Viongozi wa vyama vinavyounda Serikali ya Mseto ya Israel wamekubaliana kulivunja Bunge na kuitisha uchaguzi  mpya Aprili 2019. Baada ya mkutano wa leo Jumanne kwa sauti moja wamekubaliana kuvunja Bunge na kuitisha uchaguzi mapema baada ya muhula wa miaka minne. Hatua hiyo imefikiwa huku kukiwa na mvutano ndani ya Serikali ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu ya siasa za mlengo wa kulia. Netanyahu amekabiliwa na shinikizo la madai ya ufisadi, huku waendesha mashtaka wakimtafutia sababu za kumfungulia mashtaka tokea mwanzoni wa mwaka. Hata hivyo, ripoti zinasema kuwa Mkuu wa zamani wa Jeshi la Ulinzi la Israeli (IDF), Benny Gantz, anajiandaa kugombea kama mgombea binafsi hali ambayo inaweza kusababisha ugumu wa kutabiri matokeo. Netanyahu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Likuda amehudumu kama Waziri Mkuu wa Israel tangu 2009 mpaka sasa.