Posts

Showing posts from December 10, 2018

Kamishna TRA ‘atangaza’ ajira kiaina

Image
              Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA), Charles Kichere, amesema mamlaka hiyo ina  upungufu wa rasilimali watu 1,930 hali inayosababisha ucheleweshwaji wa ukusanyaji kodi na kutofungua ofisi zao katika baadhi ya wilaya na kuifanya serikali kukosa mapato ya maeneo hayo. Kichere ameyasema hayo leo alipokuwa akiwasilisha taarifa ya TRA katika kikao cha Rais Dk John Magufuli na mamlaka hiyo na wakuu wa mikoa  kilichofanyika leo Jumatatu Desemba 10, jijini Dar es Salaam ambapo amesema mbali na upungufu huo pia wanahitaji nyumba 114 za wafanyakazi wa mipakani na ukarabati wa majengo 76 ya ofisi zao ili kuwapa mazingira mazuri ya kufanya kazi zao kwa ufanisi na kuongeza mapato.  Aidha, Kamishna Kichere pia ameiomba serikali kupitia upya mfumo wa ulipaji kodi kwa wafanyabiashara wadogo ili kuwasaidia kulipa kodi kwa hiari na kuwaandalia maeneo maalumu ya kufanyia biashara ili kuisaidia TRA kukusanya kodi kirahisi. “Mahakama ya kodi ina kesi

RAIS JPM awajia juu wanasiasa wanaowatetea wafanyabiashara wasiolipa kodi

Image
    Rais John Magufuli, amewajia juu wanasiasa wanaowatetea wafanyabishara wasiolipa kodi na kuwataka kuacha mara moja huku akihimiza Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), kuwakamata wafanyabiashara hao haraka iwezekanavyo. Ameyasema hayo leo Jumatatu Desemba 10, katika kikao maalumu kati yake uongozi wa TRA, na wakuu wa mikoa jijini Dar es Salaam ambapo amesema ni jukumu la kila Mtazania kulipa kodi. “Kuna taarifa ya baadhi ya wafanyabashara kutetewa na wanasiasa, kwa hiyo Meneja wa TRA anamuachia, ukweli huo upo mimi  ndiyo Mwenyekiti wa chama ninakwambia mshike. “Baadhi yawafanyabiashara wameendelea kukwepa kodi kwa ujanja wa kuendeleza shughuli zauendeshaji, TRA kama kampuni kila siku inapata hasara kwanini isifungwe? Sisi hatuhitaji wawekezaji wanaopata hasara kila mwaka maana yake hiyo shughuli imemshinda,” amesema. Aidha, amesema kuwa suala la kukusanya kodiha lina chama na kwamba ifike mahali watu wote walipe kwani wasipokusanya kodi nchi haitafika mahali.

Shahidi abanwa mshtakiwa kutoa rushwa kwa waziri

Image

Magufuli atoa vitambulisho maalumu kwa wafanyabiashara wadogo

Image
                    Rais John Magufuli, amezindua vitambulisho maalumu 670,000 kwa ajili ya wafanyabiashara wadogo wadogo ili viwasaidie kuzitambulisha biashara zao. Rais Magufuli amegawa vitambulisho hivyo leo Jumatatu Desemba 10, alipokuwa katika mkutano wake na viongozi wa Mamlaka yaMapato (TRA) na wakuu wa mikoa ambapo amesema vitambulisho hivyo ni maalumu kwa wafanyabiashara ambao mtaji wao hauzidi Sh milioni nne. Baada ya kugawa vitambulisho hivyo maalumu kwa wakuu wa mikoa ili wakawapatie wafanyabiashara katika maeneo yao, Rais Magufuli ametaka wafanyabiashara hao wasisumbuliwe na mtu yeyote. “Nimefikia hatua ya kutoa vitambulisho hivyo mimi mwenyewe kwa sababu nimeona mamlaka husika inachelewesha na wafanyabiashara wadogo wanaendelea kusumbuliwa. Rais Magufuli amesema vitambulisho hivyo viko 670,000 na kila mkuu wa mkoa atapewa vitambulisho 25, 000 ili wakavigawe kwa wafanyabiashara wa maeneo yao na fedha watakazopewa wakazilipe TRA. “Vitambulisho hivi na

Mikopo mingi chechefu inatokana na wafanyakazi wa benki wasio waaminifu’

Image
                Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Profesa Florens Luoga, amebainisha sababu za benki kutokopesha linatokana na benki zenyewe kutokuwa na wafanyakazi waaminifu kwa kuruhusu wakopaji wasiokidhi vigezo na kusababisha mikopo chechefu. Kutokana na hali hiyo, amesema BoT imechukua jukumu la kufuatilia kuajiriwa kwa watumishi hao pamoja na mambo mengine.                               Profesa Luoga amesema hayo leo Jumatatu Desemba 10, katika mkutano wa Rais John Magufuli na uongozi wa Mamlaka ya Mapato nchini (TRA). “Ni kweli benki zinapaswa kuwa huru lakini BoT inapaswa kuangalia mwenendo wao, kwa mfano kuna wakati mikopo ilikuwa haitolewi, BoT imechukua jukumu na imekuwa ikikaa chini na benki nchini kutathmini kwanini mikopo haitolewi na mara nyingi majibu na kwamba benki inaogopa hasara kwa sababu watu hawajulikani lakini BoT imechukua jukumu kuhakikisha watu wanajulikana. “Pia kumekuwa na tatizo la rushwa, wakopaji wengine wabovu