Posts

Showing posts from January 17, 2019

CAG ashindwa kunyamaza, amjibu Spika

Image
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za serikali (CAG), Prof. Mussa Asad amesema kuwa ameitika wito wa kisheria kutoka wa Kamati ya Kudumu ya Bunge, Maadili na Madaraka ya Bunge uliyomtaka kwa ajili ya mahojiano ifikapo January 21 mwaka huu.

HABARI KUBWA LEO IJUMAA 18/1/2019

Image

Tundu Lissu anyoosha maelezo kuhusu kugombea Urais 2020

Image
Mwanasiasa wa upinzani nchini, Tundu Lissu ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki amesisitiza kuwa iwapo chama chake kitamteua kuwa mgombe wa urasi 2020 yupo tayari. Mwanasheria huyo Mkuu wa CHADEMA akizungumza na Idhaa ya Kiswahili ya BBC amesema yeye kugombea au kutogombea inategemea na maamuzi kutoka kwenye vikao vya chama chake. "Nimesema na ninaomba nirudie tena, kama chama changu na vyama tunavyoshirikiana navyo na Watanzania wanaotuunga mkono watasema kwamba mimi ninafaa, nipo tayari kufanya hivyo," amesema Tundu Lissu. Kwa sasa Tundu Lissu yupo katika ziara nchini Uingereza, moja ya lengo la ziara yake hiyo ni kueleza tukio la kushambuliwa na kujeruhiwa vibaya kwa risasi Septemba 17, 2017.

je, aacha mtoto mwema? Baba Mzazi wa Alikiba afariki Dunia

Image
Baba wa msanii wa msanii wa Bongo Fleva, AliKiba amefariki dunia. Mzee Saleh Kiba mefariki Dunia alfajiri ya leo katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alipokuwa amelazwa. Alikiba anafikwa na msiba wakati akiwa kwenye mchakato wa kuhakikisha kinywaji chake cha Mo Faya kinaingia sokoni.

Kangi Lugola afanya haya

Image
RAMADHAN HASSAN-DODOMA WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola ametengua uteuzi wa makanda watatu wa polisi kutokana na kushindwa kutii maagizo yake pamoja na rushwa. Waliotenguliwa kuwa makamanda wa polisi wa mikoa ni makamanda wa polisi wa mikoa ya polisi ya Ilala (Salum Hamduni) na Temeke (Emmanuel Lukula) na Kamanda wa Mkoa wa Arusha, Ramadhan Ng’azi. Akizungumza na waandishi wa habari  Dodoma jana, Waziri Lugola alisema kabla ya kuchukua uamuzi huo, juzi alikutana na wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama  ambao waliwapa maelekezo ya nini wanatakiwa kufanya kuhakikisha mambo yanakwenda vizuri. Alisema   suala la makamanda wa polisi ambao wamesimamishwa imetokana na kushindwa kusimamia suala la rushwa jambo ambalo wameshindwa kulifanyia kazi eti kwa sababu yeye (aliyetoa agizo) ni mwanasiasa. “Kuna maelekezo nilitoa lakini kuna mikoa inabeza maelekezo hayo na maagizo hayafanyiwi kazi na mrejesho ninaopata ni kwamba maelekezo haya  hayafanyiwi kazi kw

Wapinzani: Spika tengua kauli yako

Image
SARAH MOSES -DODOMA KAMBI ya Upinzani Bungeni, imemtaka Spika wa Bunge, Job Ndugai, kutengua uamuzi wake wa kusimamisha vikao vya kamati za Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) na Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa ( LAAC ). Akizungumza na waandishi wa habari  jijini Dodoma jana, Mwakilishi wa Kambi ya Upinzani, John Mnyika alisema kauli aliyoitoa spika siyo ya Bunge, bali ni yake binafsi. “Haiwezekani mgogoro wa Spika na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Musa Assad, ukasimamisha mambo mengine ya  bunge kuendelea. “Kama kamati tunamtaka spika abadilishe uamuzi wake kwa kamati hizi mbili na awezeshe kamati hizo kukutana kabla ya tarehe 25 mwezi huu,”alisema Mnyika na kuongeza: “Tumesikia spika amesimamisha kamati hizo kwa kuwa CAG ameitwa kwenye Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge Januari 21, mwaka huu  kwa kile alichokiita mgogoro wa  CAG na Bunge … kauli hiyo siyo ya Bunge ila ni yake binafsi”. Alisema uamuzi alioutangaza Spika

Katibu baraza la ardhi kortini

Image
BENJAMIN MASESE MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Geita imehukumiwa Katibu wa Baraza la Kata la Nyamboge, Theleza Barnabas, kifungo cha miaka mitano au kulipa sh 200,000  kila kosa  kwa kupatikana na  hatia  ya kuomba na kupokea rushwa. Alilipa faini na kuachiwa.  Akitoa hukumu,  Hakimu  wa mahakama hiyo, Jovith Kato alisema  mahakama ilizingatia ushahidi wa jamuhuri na ushahidi wa utetezi.  Awali,  Mwendesha Mashitaka wa Takukuru, Dennis Lekayo alidai   Septemba  13, 2018 katika Kata ya Nyamboge  wilayani Geita, mshitakiwa aliomba rushwa ya Sh 200,000 kutoka kwa Sanda Magohe   amsaidie kupata ushindi kwenye shauri la ardhi namba 01/2018 dhidi ya Dotto Maonyole lilokuwa linasikilizwa na Baraza la Kata ya Nyamboge. Baada ya kuombwa rushwa hiyo,   Sanda ambaye alikuwa ni mlalamikaji katika shauri hilo, aliamua kutoa taarifa hiyo kwa Takukuru Mkoa wa Geita ambako mtego uliandaliwa kwa kutumia fedha za mtego. Alisema Septemba 20, 2018 Sanda alimpelekea fedha h

SOMA HIYO!:Wananchi wahamasishwa kubangua korosho

Image
HADIJA OMARY-LINDI MKUU wa Wilaya ya Lindi, Shahibu Ndemanga, amewataka wajasiriamali wilayani hapa kuchangamkia fursa ya ubanguaji wa korosho iliyotolewa na Serikali ili waweze kujikwamua kiuchumi. Ndemanga aliyasema hayo mjini hapa jana alipokuwa akifunga mafunzo ya ubanguaji bora wa korosho yaliyotolewa na Shirika la Kuhudumia Viwanda Vidogo Vidogo (Sido), Mkoa wa Lindi. Ndemanga alisema kwamba, Serikali ilipoamua korosho zote zibanguliwe ndani ya nchi, ilikuwa na lengo la kuinua uchumi wa wananchi wake na kwamba wananchi wanatakiwa kutumia fursa hiyo ili kuinua uchumi wao. “Uamuzi wa Sido wa kuwakusanya wajasiriamali na kuwapa mafunzo ya ubanguaji bora wa korosho ni kitendo cha kizalendo kwani kitawafanya wajasiriamali kuanzisha viwanda vidogo vidogo vya ubanguaji  vitakavyowaongezea kipato,” alisema Ndemanga. Naye Ofisa Uendelezaji Mafunzo kutoka Sido, Aizack Daniely, alisema  katika mafunzo hayo ya siku tano yenye lengo la kuongeza kasi ya uongezaji wa thamani katika zao la

Kidato cha kwanza waruhusiwa kuvaa sare za shule ya msingi

Image
  Kidato cha kwanza waruhusiwa kuvaa sare za shule ya msingi Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Ruth Msafiri ametoa ruhusa kuvaa sare za elimu ya msingi kwa wanafunzi ambao wamefanikiwa kufaulu elimu ya msingi na kushindwa kujiunga na elimu ya Sekondari kutokana na wazazi kushindwa kukamilisha mahitaji hayo. Ametoa ruhusa hiyo alipotembelea katika shule ya Sekondari Maheve iliyopo katika Kata ya Ramadhani pamoja na shule ya Sekondari Joseph Mbeyela zilizopo halmashauri ya mji wa Njombe na kupata taarifa ya baadhi ya wanafunzi kushindwa kufika shuleni kutokana na kukosa baadhi ya mahitaji kama sare za shule. “Hawa wanafunzi si walikuwa wanasoma, sasa hawa watoto waje na uniform zao za shule za msingi waje na chakula wakati wazazi wanaendelea kukamilisha