Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli
ameweka Jiwe la Msingi Mradi wa Ujenzi Daraja Jipya na Barabara ya Aga
Khan Hadi Coco Beach.
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wengine
wakipata maelezo toka kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini
(TANROADS) Mhandisi Robert Mfugale kuhusu Mradi wa Ujenzi wa Daraja
Jipya la Selanderna Barabara unganishi ya Km 6.23 toka Hospitali ya Aga
Khan hadi ufukwe wa Coco Beach jijini Dar es salaam leo Desemba 20, 2018
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipongezana na Balozi wa
Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Cho Tae-ick baada ya kuweka jiwe la Msingi
la Mradi wa Ujenzi wa Daraja Jipya la Selander na Barabara unganishi ya
Km 6.23 toka Hospitali ya Aga Khan hadi ufukwe wa Coco Beach jijini Dar
es salaam leo Desemba 20, 2018. Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Mama
Janeth Magufuli na viongozi wengine wanashuhudia
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akishirikiana na Balozi wa
Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Cho Tae-ick kufunua pazia kuashiria
kuwekwa kwa jiwe la Msingi la Mradi wa Ujenzi wa Daraja Jipya la
Selander na Barabara unganishi ya Km 6.23 toka Hospitali ya Aga Khan
hadi ufukwe wa Coco Beach jijini Dar es salaam leo Desemba 20, 2018.
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Mama Janeth Magufuli na viongozi
wengine wanashuhudia
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea kwenye sherehe za
kuweka jiwe la Msingi Mradi wa Ujenzi wa Daraja Jipya la Selander na
Barabara unganishi ya Km 6.23 toka Hospitali ya Aga Khan hadi ufukwe wa
Coco Beach jijini Dar es salaam leo Desemba 20, 2018
Serikali ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), imekemea ushawishi unaotolewa na kanisa Katoliki unaodai kuwa wanajua kiongozi aliyeshinda katika uchaguzi wa rais. Barnabe Kikaya Bin Karubi ambaye ni msemaji wa 'Common front for the Congo', ameiambia BBC kuwa "Jambo linalofanywa na kanisa ni kitu ambacho hakikubaliki, ni sawa na kuwaandaa watu kufanya mapinduzi". Serikali ya mseto imesisitiza kwamba ni Tume ya uchaguzi peke yake ndio inaweza kutangaza matokeo ya uchaguzi. Matokeo ya uchaguzi wa urais DRC 'kuchelewa' Huduma ya intaneti yafungwa DR Congo siku moja baada ya uchaguzi Wagombea wa upinzani walalamikia dosari uchaguzi DRC Kanisa Katoliki, ambalo lina ushawishi mkubwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, limesema kuwa kuna mshindi wazi wa urais katika uchaguzi uliofanyika Jumapili, kwa mujibu wa matokeo ambao wamefanikiwa kuyaona. Maaskofu wa kanisa hilo wamewataka watawala nchini humo kuwa wakweli na kutangaza matokeo hayo karib...
NAIBU Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi, Dk. Angelina Mabula amewavua nyadhifa wakuu wa Idara ya Ardhi katika Manispaa ya Kigoma Ujiji na Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kwa kushindwa kutekeleza majukumu yao ya kazi ipasavyo. Waliovuliwa nyadhifa hizo ni Mkuu wa Idara ya Ardhi wa Manispaa ya Kigoma, Brown Nziku, Mkuu wa Idara ya Ardhi Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma, Emanuel Magembe na Ofisa Ardhi Mteule, Paul Misuzi. Mabula alifanya uamuzi huo Januari 3, mwaka huu akiwa mkoani hapa baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika Manispaa ya Kigoma Ujiji na Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma. Alifikia uamuzi huo baada ya watendaji hao kushindwa kusimamia maagizo na maelekezo yaliyotolewa tangu mwaka juzi kuhusu ukusanyaji wa kodi ya ardhi, uingizaji wa wamiliki wa viwanja na mashamba kwenye mfumo wa malipo kwa njia ya kielekroniki wa ardhi na utoaji wa hati za madai kwa wadaiwa sugu wa kodi ya ardhi. Mabula alisema pamoja na barua iliyoandikwa na Kamishna wa Ardhi Msaidiz...
Fahamu yote yaliyojiri katika Magazeti ya Tanzania leo ALHAMISI january 17, 2019. Hapa unapata habari zote zilizopewa uzito katika kurasa za mbele na kurasa za nyuma za habari za michezo na burudani.
Comments