Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli
ameweka Jiwe la Msingi Mradi wa Ujenzi Daraja Jipya na Barabara ya Aga
Khan Hadi Coco Beach.
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wengine
wakipata maelezo toka kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini
(TANROADS) Mhandisi Robert Mfugale kuhusu Mradi wa Ujenzi wa Daraja
Jipya la Selanderna Barabara unganishi ya Km 6.23 toka Hospitali ya Aga
Khan hadi ufukwe wa Coco Beach jijini Dar es salaam leo Desemba 20, 2018
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipongezana na Balozi wa
Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Cho Tae-ick baada ya kuweka jiwe la Msingi
la Mradi wa Ujenzi wa Daraja Jipya la Selander na Barabara unganishi ya
Km 6.23 toka Hospitali ya Aga Khan hadi ufukwe wa Coco Beach jijini Dar
es salaam leo Desemba 20, 2018. Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Mama
Janeth Magufuli na viongozi wengine wanashuhudia
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akishirikiana na Balozi wa
Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Cho Tae-ick kufunua pazia kuashiria
kuwekwa kwa jiwe la Msingi la Mradi wa Ujenzi wa Daraja Jipya la
Selander na Barabara unganishi ya Km 6.23 toka Hospitali ya Aga Khan
hadi ufukwe wa Coco Beach jijini Dar es salaam leo Desemba 20, 2018.
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Mama Janeth Magufuli na viongozi
wengine wanashuhudia
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea kwenye sherehe za
kuweka jiwe la Msingi Mradi wa Ujenzi wa Daraja Jipya la Selander na
Barabara unganishi ya Km 6.23 toka Hospitali ya Aga Khan hadi ufukwe wa
Coco Beach jijini Dar es salaam leo Desemba 20, 2018
KESI ya Kiongozi wa ACT Wazalendo na wenzake wa vyama 10 vya upinzani ya kupinga muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa iliyopangwa kusikilizwa na jopo la majaji watatu wa Mahakama Kuu leo majira ya saa 3 asubuhi, limehamishiwa kwa Jaji mmoja. Shauri la kesi hiyo lilipangwa kusikilizwa na Majaji; Barke Sehel (kiongozi wa jopo), Benhajo Masoud na Salma Maghimbi, lakini limekwama baada ya wajibu maombi (Serikali) kuwasilisha pingamizi la awali wakiitaka Mahakama hiyo ilitupilie mbali. Aidha, kutokana na pingamizi hilo, Mahakama imesitisha usikilizwaji wa shauri la msingi na badala yake imeamua kuanza kusikiliza pingamizi ambapo imepanga kusikiliza pingamizi hilo na jaji Masoud katika chemba kuanzia saa 4:00, asubuhi. Zitto na Viongozi wa Upinzani kwenye Kesi Yao Mahakama Kuu Leo
WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isaak Kamwelwe, amesimamisha likizo za marubani wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) katika kipindi cha mwisho wa mwaka. Amesema marubani wa ATCL ambao wameshaanza likizo wanapaswa kurudi kazini na kuendelea na kazi ya kutoa huduma kwa wananchi. Kamwelwe aliyasema hayo jana muda mfupi baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) akitokea mkoani Mbeya kwenye ukaguzi wa Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Songwe (SIA). Alisema wafanyakazi wa Mamalaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) nao hawapaswi kwenda likizo kipindi hiki cha mwisho wa mwaka bali wanapaswa kuhakikisha magari yaendayo mikoani hayapandishi nauli. "Hakuna Mtanzania atakayepata shida ya kusafiri kipindi hiki cha sikukuu. Tumejipanga kusafirisha abiria hadi usiku," alisema Waziri Kamwelwe. Alisema maofisa wa Sumatra wanapaswa kuhakikisha abiria hawaonewi wala kusumbuliwa na wenye mabasi hususani eneo l
Comments