Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli
ameweka Jiwe la Msingi Mradi wa Ujenzi Daraja Jipya na Barabara ya Aga
Khan Hadi Coco Beach.
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wengine
wakipata maelezo toka kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini
(TANROADS) Mhandisi Robert Mfugale kuhusu Mradi wa Ujenzi wa Daraja
Jipya la Selanderna Barabara unganishi ya Km 6.23 toka Hospitali ya Aga
Khan hadi ufukwe wa Coco Beach jijini Dar es salaam leo Desemba 20, 2018
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipongezana na Balozi wa
Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Cho Tae-ick baada ya kuweka jiwe la Msingi
la Mradi wa Ujenzi wa Daraja Jipya la Selander na Barabara unganishi ya
Km 6.23 toka Hospitali ya Aga Khan hadi ufukwe wa Coco Beach jijini Dar
es salaam leo Desemba 20, 2018. Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Mama
Janeth Magufuli na viongozi wengine wanashuhudia
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akishirikiana na Balozi wa
Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Cho Tae-ick kufunua pazia kuashiria
kuwekwa kwa jiwe la Msingi la Mradi wa Ujenzi wa Daraja Jipya la
Selander na Barabara unganishi ya Km 6.23 toka Hospitali ya Aga Khan
hadi ufukwe wa Coco Beach jijini Dar es salaam leo Desemba 20, 2018.
Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Mama Janeth Magufuli na viongozi
wengine wanashuhudia
Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiongea kwenye sherehe za
kuweka jiwe la Msingi Mradi wa Ujenzi wa Daraja Jipya la Selander na
Barabara unganishi ya Km 6.23 toka Hospitali ya Aga Khan hadi ufukwe wa
Coco Beach jijini Dar es salaam leo Desemba 20, 2018
Na ANDREW MSECHU-DAR ES SALAA KITUO kikubwa cha biashara cha kimataifa kinatarajiwa kujengwa katika eneo la Stendi ya Mabasi ya Ubungo, ujenzi utakaoanza Januari mwakani na kuchukua miezi 18 kukamilika. Akizungumza na MTANZANIA jana, Meneja wa Mauzo wa Kampuni ya East Africa Commercial & Logistics Center Tom Zhang, alisema kitakapokamilika kituo hicho kinatarajiwa kuwa namba moja kwa nchi za Afrika Mashariki. Alisema kwa sasa tayari wana vituo viwili vya aina hiyo, cha kwanza kikiitwa Dragon Mall ambacho kipo nchini Dubai na kingine kikiitwa Yiwu City Mall nchini China. “Kituo hiki kitakuwa maalumu kwa ajili ya kuingiza bidhaa kutoka nje na kuuza bidhaa kwenda nje. Kutakuwa karibu na kila kitu kinachohitajika kwa ajili ya biashara za kimataifa. “Hii ina maana kwamba kikishakamilika, hakutakuwa na sababu ya mfanyabiashara wa Tanzania kusafiri kwenda China au nje ya nchi kununua bidhaa na kuzileta nchini. Safari hizo zinagharimu muda mwingi na gharama kub...
Comments