Nyumba zaidi ya 300 zimezama na maji baada ya kukumbwa na mafuriko
katika Kata ya Magaoni, hivyo kusababisha wakazi wake kuhama makazi yao.
Tukio lilo lilitokea usiku wa kuamkia jana majira ya saa 7:00 usiku baada ya mvua kubwa kunyesha usiku kucha.
Mwenyekiti wa Kata ya Magaoni, Kassim Abdallah, ambaye pia nyumba yake
imezama, alisema kuwa mvua iliyonyesha usiku wakuamkia jana, imeacha
hasara kubwa kwa wakazi wa kata hiyo kutokana na kuzingirwa na maji,
huku mali mbalimbali zikiharibika.
Alisema mvua hiyo ilianza kunyesha wakati huo mpaka saa 2:00 asubuhi,
hivyo kusababisha idadi kubwa ya wananchi kukosa mahali pa kuishi, hivyo
kuhamia katika shule na wengine kuhifadhiwa kwa ndugu na jamaa zao.
Abdallah alisema kata hiyo ni mpya kwa kuwa mwanzo ilikuwa sehemu ya kata ya Mabawa kabla ya kugawanywa.
Alisema sababu kubwa ya mafuriko hayo ni kukosekana kwa mifereji ya
kutosha, hivyo kushindwa kuruhusu maji kutiririka kwa urahisi.
Mwenyekiti huyo alisema Diwani wa Kata hiyo, Mohamed Rajabu, baada ya
kuchaguliwa mwaka 2015 alijitahidi kuhakikisha mifereji inajengwa
lakini iliyopo haitoshelezi mahitaji ndiyo maana imekuwa rahisi kutokea
mafuriko.
Kutokana na athari hiyo, aliiomba Halmashauri ya Jiji la Tanga kutenga
fedha kwa ajili ya mifereji, vinginevyo maafa yanaweza kuwa makubwa
zaidi.
Naye Diwani Rajabu alisema mvua hiyo imesababisha mafuriko makubwa na
kwamba mpaka sasa wananchi hawana mahali pa kuishi na wamezikimbia
nyumba zao huku vyombo vyote vikiwa vimeharibika.
Alisema kuwa ili kuondoa tatizo hilo, alisema ni lazima Halmashauri ya
Jiji la Tanga ipange bajeti kwa ajili ya kutengeneza mifereji
ya kupitisha maji katika kata hiyo, vinginevyo kunawezekana kutokea
maafa makubwa zaidi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ameweka Jiwe la Msingi Mradi wa Ujenzi Daraja Jipya na Barabara ya Aga Khan Hadi Coco Beach. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wengine wakipata maelezo toka kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) Mhandisi Robert Mfugale kuhusu Mradi wa Ujenzi wa Daraja Jipya la Selanderna Barabara unganishi ya Km 6.23 toka Hospitali ya Aga Khan hadi ufukwe wa Coco Beach jijini Dar es salaam leo Desemba 20, 2018 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipongezana na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Cho Tae-ick baada ya kuweka jiwe la Msingi la Mradi wa Ujenzi wa Daraja Jipya la Selander na Barabara unganishi ya Km 6.23 toka Hospitali ya Aga Khan hadi ufukwe wa Coco Beach jijini Dar es salaam leo Desemba 20, 2018. Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Mama Janeth Magufuli na viongozi wengine wanashuhudia Rais wa Jamhuri ...
Mlezi wa timu ya taifa ya soka ya vijana chini ya miaka 17, Serengeti Boys, Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dkt. Reginald Mengi, amewapongeza wachezaji hao kwa ubingwa wa COSAFA walioutwaa nchini Botswana. Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dkt. Reginald Mengi akipokea kombe la COSAFA kutoka kwa nahodha wa Serengeti Boys Michael Morris. Dkt. Mengi ametoa pongezi hizo leo Desemba 20, 2018 katika hafla ya chakula cha mchana alioyowaandalia vijana hao pamoja na viongozi wa TFF na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakiongozwa na Waziri Harrison Mwakyembe. Akiongea katika hafla hiyo Dkt. Mengi amesema, ''nyinyi mlizaliwa washindi na siku zote nalisema hilo, nawashukuru vijana wangu kwa kutekeleza ahadi ya kurudi na kombe hili kama mlezi wenu nimejisikia vizuri sana'', amesema. Katika hafla ya ch...
MELI za mizigo za MV Ruvuma na MV Njombe zimeongeza mwamko wa biashara, hasa usafirishaji makaa ya mawe katika bandari za Ziwa Nyasa. Makaa ya mawe husafirishwa kutoka Bandari ya Ndumbi wilayani Nyasa hadi katika Bandari ya Kiwira iliyopo wilayani Kyela. Akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea bandari za Itungi na Kiwira juzi, Meneja wa bandari za Ziwa Nyasa, Abed Gallus alisema meli hizo zenye uwezo wa kubeba tani 1,000 kila moja zimegharimu Sh bilioni 11 na zilianza kutengenezwa mwaka 2015 na kukamilika mwaka jana. “Meli za mizigo na ujenzi wa meli ya abiria (MV Mbeya) ni miradi ya maendeleo tuliyoanza kuitekeleza mwaka 2015 ili kuongeza ufanisi wa bandari za Ziwa Nyasa. “Tunashukuru mwamko wa wateja umeanza kuwa mzuri, hasa wale wanaojihusisha na biashara ya makaa ya mawe,” alisema Gallus. Alisema meli hizo tayari zimeshafanya safari saba hadi sasa na kati ya hizo, nne zilikuwa za majaribio na tatu za kibiashara ambazo zilifanywa kati ya Se...
Comments