Watu
wengi hupendelea kutumia maji ya moto kuoga pale hali ya hewa
inapobadilika na kuwa ya baridi au wakati mwingine mtu anaumwa hivyo
anatumia maji ya moto.
Sehemu kama Dar es Salaam ni mara cheche utakuta wakazi wake wanaogea maji ya moto kutokana na hali ya joto katika jiji hilo.
Lakini
kwa ajili ya urembo na afya ya ngozi, maji ya moto yanatajwa kuwa ni
kitu muhimu sana kama vilivyo vipodozi vingine vinavyoisaida ngozi yako
kuwa nyororo.
Hizi hapa ni baadhi ya faida zitokanazo na matumizi ya maji ya moto angalau mara tatu kwa wiki
Kulainisha na kutunza ngozi
Maji
ya moto husaidia kulainisha ngozi yako tofauti na ukitumia maji ya
baridi. Maji ya moto hasa yaliyo katika jakuzi ambapo utatumia muda
mrefu kidogo ngozi yako ikiwa kwenye maji, husaidia kuilainisha ngozi
yako na kuiweka katika hali nzuri.
Usingizi
Kama
huwa unapata matatizo kupata usingizi usiku, amka oga kwa kutumia maji
ya moto kwani husaidia kulainisha misuli ya mwili wako na itakaa sawa na
utaweza kupata usinngizi.
Kukuweka katika hali nzuri
Kuna
wakati mwingine mtu hujisikia uchovu wa mwili na kutotaka kufanya
chochote (Off mood). Ukioga kwa maji ya moto yatakusaida kukuondolea
uchovu na utajisikia mwenye nguvu na upo tayari kukabiliana na
changamoto za siku.
Kuchangamsha ubongo
Unapooga kwa kutumia maji ya moto husaidia kuchangamsha ubongo na kuufanya uweze kufanyakazi kwa ufanisi na kwa haraka zaidi.
Kushusha shinikizo la damu
Ukiachanna
na masuala ya urembo, kuoga maji ya moto kunatajwa kuwa ni njia ya
haraka ya kusaidia kushusha shinikizo la damu. Tafiti zinaonyesha kuwa
mtu mwenye shinikizo la damu la kupanda, akioga kwa maji ya moto
husaidia kushusha.
Kusaidia mzunguko wa damu
Ukioga
kwa kutumia maji ya moto husaidia kusisimu na kuitanua mishipa ya damu
hivyo kuwezesha damu kuwa na mzunguko mzuri mwilini.
TAHADHARI Licha ya kuwa maji ya moto ni mazuri kiafya, unashauriwa kuto oga kwa maji ya moto sana kwani huathiri ngozi.
Serikali ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), imekemea ushawishi unaotolewa na kanisa Katoliki unaodai kuwa wanajua kiongozi aliyeshinda katika uchaguzi wa rais. Barnabe Kikaya Bin Karubi ambaye ni msemaji wa 'Common front for the Congo', ameiambia BBC kuwa "Jambo linalofanywa na kanisa ni kitu ambacho hakikubaliki, ni sawa na kuwaandaa watu kufanya mapinduzi". Serikali ya mseto imesisitiza kwamba ni Tume ya uchaguzi peke yake ndio inaweza kutangaza matokeo ya uchaguzi. Matokeo ya uchaguzi wa urais DRC 'kuchelewa' Huduma ya intaneti yafungwa DR Congo siku moja baada ya uchaguzi Wagombea wa upinzani walalamikia dosari uchaguzi DRC Kanisa Katoliki, ambalo lina ushawishi mkubwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, limesema kuwa kuna mshindi wazi wa urais katika uchaguzi uliofanyika Jumapili, kwa mujibu wa matokeo ambao wamefanikiwa kuyaona. Maaskofu wa kanisa hilo wamewataka watawala nchini humo kuwa wakweli na kutangaza matokeo hayo karib...
NAIBU Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi, Dk. Angelina Mabula amewavua nyadhifa wakuu wa Idara ya Ardhi katika Manispaa ya Kigoma Ujiji na Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kwa kushindwa kutekeleza majukumu yao ya kazi ipasavyo. Waliovuliwa nyadhifa hizo ni Mkuu wa Idara ya Ardhi wa Manispaa ya Kigoma, Brown Nziku, Mkuu wa Idara ya Ardhi Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma, Emanuel Magembe na Ofisa Ardhi Mteule, Paul Misuzi. Mabula alifanya uamuzi huo Januari 3, mwaka huu akiwa mkoani hapa baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika Manispaa ya Kigoma Ujiji na Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma. Alifikia uamuzi huo baada ya watendaji hao kushindwa kusimamia maagizo na maelekezo yaliyotolewa tangu mwaka juzi kuhusu ukusanyaji wa kodi ya ardhi, uingizaji wa wamiliki wa viwanja na mashamba kwenye mfumo wa malipo kwa njia ya kielekroniki wa ardhi na utoaji wa hati za madai kwa wadaiwa sugu wa kodi ya ardhi. Mabula alisema pamoja na barua iliyoandikwa na Kamishna wa Ardhi Msaidiz...
Fahamu yote yaliyojiri katika Magazeti ya Tanzania leo ALHAMISI january 17, 2019. Hapa unapata habari zote zilizopewa uzito katika kurasa za mbele na kurasa za nyuma za habari za michezo na burudani.
Comments