Watu
wengi hupendelea kutumia maji ya moto kuoga pale hali ya hewa
inapobadilika na kuwa ya baridi au wakati mwingine mtu anaumwa hivyo
anatumia maji ya moto.
Sehemu kama Dar es Salaam ni mara cheche utakuta wakazi wake wanaogea maji ya moto kutokana na hali ya joto katika jiji hilo.
Lakini
kwa ajili ya urembo na afya ya ngozi, maji ya moto yanatajwa kuwa ni
kitu muhimu sana kama vilivyo vipodozi vingine vinavyoisaida ngozi yako
kuwa nyororo.
Hizi hapa ni baadhi ya faida zitokanazo na matumizi ya maji ya moto angalau mara tatu kwa wiki
Kulainisha na kutunza ngozi
Maji
ya moto husaidia kulainisha ngozi yako tofauti na ukitumia maji ya
baridi. Maji ya moto hasa yaliyo katika jakuzi ambapo utatumia muda
mrefu kidogo ngozi yako ikiwa kwenye maji, husaidia kuilainisha ngozi
yako na kuiweka katika hali nzuri.
Usingizi
Kama
huwa unapata matatizo kupata usingizi usiku, amka oga kwa kutumia maji
ya moto kwani husaidia kulainisha misuli ya mwili wako na itakaa sawa na
utaweza kupata usinngizi.
Kukuweka katika hali nzuri
Kuna
wakati mwingine mtu hujisikia uchovu wa mwili na kutotaka kufanya
chochote (Off mood). Ukioga kwa maji ya moto yatakusaida kukuondolea
uchovu na utajisikia mwenye nguvu na upo tayari kukabiliana na
changamoto za siku.
Kuchangamsha ubongo
Unapooga kwa kutumia maji ya moto husaidia kuchangamsha ubongo na kuufanya uweze kufanyakazi kwa ufanisi na kwa haraka zaidi.
Kushusha shinikizo la damu
Ukiachanna
na masuala ya urembo, kuoga maji ya moto kunatajwa kuwa ni njia ya
haraka ya kusaidia kushusha shinikizo la damu. Tafiti zinaonyesha kuwa
mtu mwenye shinikizo la damu la kupanda, akioga kwa maji ya moto
husaidia kushusha.
Kusaidia mzunguko wa damu
Ukioga
kwa kutumia maji ya moto husaidia kusisimu na kuitanua mishipa ya damu
hivyo kuwezesha damu kuwa na mzunguko mzuri mwilini.
TAHADHARI Licha ya kuwa maji ya moto ni mazuri kiafya, unashauriwa kuto oga kwa maji ya moto sana kwani huathiri ngozi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ameweka Jiwe la Msingi Mradi wa Ujenzi Daraja Jipya na Barabara ya Aga Khan Hadi Coco Beach. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli na viongozi wengine wakipata maelezo toka kwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Barabara nchini (TANROADS) Mhandisi Robert Mfugale kuhusu Mradi wa Ujenzi wa Daraja Jipya la Selanderna Barabara unganishi ya Km 6.23 toka Hospitali ya Aga Khan hadi ufukwe wa Coco Beach jijini Dar es salaam leo Desemba 20, 2018 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akipongezana na Balozi wa Jamhuri ya Korea nchini Mhe. Cho Tae-ick baada ya kuweka jiwe la Msingi la Mradi wa Ujenzi wa Daraja Jipya la Selander na Barabara unganishi ya Km 6.23 toka Hospitali ya Aga Khan hadi ufukwe wa Coco Beach jijini Dar es salaam leo Desemba 20, 2018. Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Mama Janeth Magufuli na viongozi wengine wanashuhudia Rais wa Jamhuri ...
Mlezi wa timu ya taifa ya soka ya vijana chini ya miaka 17, Serengeti Boys, Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dkt. Reginald Mengi, amewapongeza wachezaji hao kwa ubingwa wa COSAFA walioutwaa nchini Botswana. Mwenyekiti Mtendaji wa Makampuni ya IPP Dkt. Reginald Mengi akipokea kombe la COSAFA kutoka kwa nahodha wa Serengeti Boys Michael Morris. Dkt. Mengi ametoa pongezi hizo leo Desemba 20, 2018 katika hafla ya chakula cha mchana alioyowaandalia vijana hao pamoja na viongozi wa TFF na Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo wakiongozwa na Waziri Harrison Mwakyembe. Akiongea katika hafla hiyo Dkt. Mengi amesema, ''nyinyi mlizaliwa washindi na siku zote nalisema hilo, nawashukuru vijana wangu kwa kutekeleza ahadi ya kurudi na kombe hili kama mlezi wenu nimejisikia vizuri sana'', amesema. Katika hafla ya ch...
MELI za mizigo za MV Ruvuma na MV Njombe zimeongeza mwamko wa biashara, hasa usafirishaji makaa ya mawe katika bandari za Ziwa Nyasa. Makaa ya mawe husafirishwa kutoka Bandari ya Ndumbi wilayani Nyasa hadi katika Bandari ya Kiwira iliyopo wilayani Kyela. Akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea bandari za Itungi na Kiwira juzi, Meneja wa bandari za Ziwa Nyasa, Abed Gallus alisema meli hizo zenye uwezo wa kubeba tani 1,000 kila moja zimegharimu Sh bilioni 11 na zilianza kutengenezwa mwaka 2015 na kukamilika mwaka jana. “Meli za mizigo na ujenzi wa meli ya abiria (MV Mbeya) ni miradi ya maendeleo tuliyoanza kuitekeleza mwaka 2015 ili kuongeza ufanisi wa bandari za Ziwa Nyasa. “Tunashukuru mwamko wa wateja umeanza kuwa mzuri, hasa wale wanaojihusisha na biashara ya makaa ya mawe,” alisema Gallus. Alisema meli hizo tayari zimeshafanya safari saba hadi sasa na kati ya hizo, nne zilikuwa za majaribio na tatu za kibiashara ambazo zilifanywa kati ya Se...
Comments