Watu
wengi hupendelea kutumia maji ya moto kuoga pale hali ya hewa
inapobadilika na kuwa ya baridi au wakati mwingine mtu anaumwa hivyo
anatumia maji ya moto.
Sehemu kama Dar es Salaam ni mara cheche utakuta wakazi wake wanaogea maji ya moto kutokana na hali ya joto katika jiji hilo.
Lakini
kwa ajili ya urembo na afya ya ngozi, maji ya moto yanatajwa kuwa ni
kitu muhimu sana kama vilivyo vipodozi vingine vinavyoisaida ngozi yako
kuwa nyororo.
Hizi hapa ni baadhi ya faida zitokanazo na matumizi ya maji ya moto angalau mara tatu kwa wiki
Kulainisha na kutunza ngozi
Maji
ya moto husaidia kulainisha ngozi yako tofauti na ukitumia maji ya
baridi. Maji ya moto hasa yaliyo katika jakuzi ambapo utatumia muda
mrefu kidogo ngozi yako ikiwa kwenye maji, husaidia kuilainisha ngozi
yako na kuiweka katika hali nzuri.
Usingizi
Kama
huwa unapata matatizo kupata usingizi usiku, amka oga kwa kutumia maji
ya moto kwani husaidia kulainisha misuli ya mwili wako na itakaa sawa na
utaweza kupata usinngizi.
Kukuweka katika hali nzuri
Kuna
wakati mwingine mtu hujisikia uchovu wa mwili na kutotaka kufanya
chochote (Off mood). Ukioga kwa maji ya moto yatakusaida kukuondolea
uchovu na utajisikia mwenye nguvu na upo tayari kukabiliana na
changamoto za siku.
Kuchangamsha ubongo
Unapooga kwa kutumia maji ya moto husaidia kuchangamsha ubongo na kuufanya uweze kufanyakazi kwa ufanisi na kwa haraka zaidi.
Kushusha shinikizo la damu
Ukiachanna
na masuala ya urembo, kuoga maji ya moto kunatajwa kuwa ni njia ya
haraka ya kusaidia kushusha shinikizo la damu. Tafiti zinaonyesha kuwa
mtu mwenye shinikizo la damu la kupanda, akioga kwa maji ya moto
husaidia kushusha.
Kusaidia mzunguko wa damu
Ukioga
kwa kutumia maji ya moto husaidia kusisimu na kuitanua mishipa ya damu
hivyo kuwezesha damu kuwa na mzunguko mzuri mwilini.
TAHADHARI Licha ya kuwa maji ya moto ni mazuri kiafya, unashauriwa kuto oga kwa maji ya moto sana kwani huathiri ngozi.
Zitto ni mchawi, kaniroga sana kashindwa na sio raia wa Tanzania- Katibu UVCCM Kigoma Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Kigoma, Agustino Matefu amepokea zaidi ya wanachama 100 kutoka chama cha ACT-Wazalendo. Katika mkutano huo wa kuwapokea wanachama hao uliofanyika jijini Dar es salaam, wanachama hao wakiwemo madiwani wamesema kuwa, wameamua kukihama chama hicho baada ya kuona kinakosa muelekeo. “Kama mnavyoona waandishi wa habari, hawa wote siwajui lakini wameamua kuniita ili waweze kujiunga na chama cha mapinduzi CCM, na hizi ni salamu kwa Zitto kwamba 2020 atafute kazi ya kufanya au arudi kwao Kongo,”amesema Matefu.
Comments