Angeline Mabula athibitisha wananchi kupokea zaidi ya Bilioni 1 kutoka Chuo cha Mzumbe

Naibu Waziri wa Ardhi Maendeleo na Makazi, Mbunge wa Jimbo la Ilemela Dk. Angeline Mabula, amethibitisha kulipwa fidia ya  Bilioni Moja na Milioni Mia Nne kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe kwa Wananchi wa Kata ya Sangabuye katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela mkoani Mwanza.

Akizungumza na Waandishi wa Habari baada ya  hafla fupi ya shukrani kutoka Chuo Kikuu cha Mzumbe, Mabula amesema kuwa wananchi 130 tayari wamepokea fidia iliyotoka na kwa sasa wako tayari kutoa ushirikiano kwa ajili ya kushirikiana nao katika ujenzi wa Tawi la chuo hicho ambapo eneo hilo lina ukubwa wa Hekari 220.

Comments

Popular posts from this blog

KESI YA ZITTO MUSWADA WA SHERIA YA VYAMA VYA SIASA YAHAMISHWA

Waziri asimamisha likizo za Marubani ATCL