INATISHA! Akutwa Amekufa Kwenye Kiroba Dar – VIDEO

MWILI wa mtu mmoja ambaye jina lake halijajulikana umekutwa ukiwa umefungwa kwenye kiroba na kutupwa kando ya barabara katika eneo la Karibu na Chuo cha Ustawi wa Jamii mkabala na Ofisi za Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), kilichopo Kijitonyama jijini Dar es Salaam.

Mtu huyo ambaye hakufahamika hata jinsia yake kutokana na namna ambavyo kiroba hicho kilikuwa kimefungwa juu na chini, anadaiwa huenda aliawa na mwili wake kutupwa ndani ya mfereji katika eneo hilo.
Global TV Online imefunga safari mpaka eneo la tukio na hii ndiyo hali halisi ilivyokuwa baada ya kuukuta mwili huo huku wananchi wa eneo hilo wakihamaki kutokana na tukio hilo la kinyama.

Comments

Popular posts from this blog

KESI YA ZITTO MUSWADA WA SHERIA YA VYAMA VYA SIASA YAHAMISHWA

Waziri asimamisha likizo za Marubani ATCL