MWILI
wa mtu mmoja ambaye jina lake halijajulikana umekutwa ukiwa umefungwa
kwenye kiroba na kutupwa kando ya barabara katika eneo la Karibu na Chuo
cha Ustawi wa Jamii mkabala na Ofisi za Kituo cha Sheria na Haki za
Binadamu (LHRC), kilichopo Kijitonyama jijini Dar es Salaam.
Mtu
huyo ambaye hakufahamika hata jinsia yake kutokana na namna ambavyo
kiroba hicho kilikuwa kimefungwa juu na chini, anadaiwa huenda aliawa na
mwili wake kutupwa ndani ya mfereji katika eneo hilo.
Global TV Online imefunga safari
mpaka eneo la tukio na hii ndiyo hali halisi ilivyokuwa baada ya kuukuta
mwili huo huku wananchi wa eneo hilo wakihamaki kutokana na tukio hilo
la kinyama.
Serikali ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), imekemea ushawishi unaotolewa na kanisa Katoliki unaodai kuwa wanajua kiongozi aliyeshinda katika uchaguzi wa rais. Barnabe Kikaya Bin Karubi ambaye ni msemaji wa 'Common front for the Congo', ameiambia BBC kuwa "Jambo linalofanywa na kanisa ni kitu ambacho hakikubaliki, ni sawa na kuwaandaa watu kufanya mapinduzi". Serikali ya mseto imesisitiza kwamba ni Tume ya uchaguzi peke yake ndio inaweza kutangaza matokeo ya uchaguzi. Matokeo ya uchaguzi wa urais DRC 'kuchelewa' Huduma ya intaneti yafungwa DR Congo siku moja baada ya uchaguzi Wagombea wa upinzani walalamikia dosari uchaguzi DRC Kanisa Katoliki, ambalo lina ushawishi mkubwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, limesema kuwa kuna mshindi wazi wa urais katika uchaguzi uliofanyika Jumapili, kwa mujibu wa matokeo ambao wamefanikiwa kuyaona. Maaskofu wa kanisa hilo wamewataka watawala nchini humo kuwa wakweli na kutangaza matokeo hayo karib...
NAIBU Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi, Dk. Angelina Mabula amewavua nyadhifa wakuu wa Idara ya Ardhi katika Manispaa ya Kigoma Ujiji na Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kwa kushindwa kutekeleza majukumu yao ya kazi ipasavyo. Waliovuliwa nyadhifa hizo ni Mkuu wa Idara ya Ardhi wa Manispaa ya Kigoma, Brown Nziku, Mkuu wa Idara ya Ardhi Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma, Emanuel Magembe na Ofisa Ardhi Mteule, Paul Misuzi. Mabula alifanya uamuzi huo Januari 3, mwaka huu akiwa mkoani hapa baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika Manispaa ya Kigoma Ujiji na Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma. Alifikia uamuzi huo baada ya watendaji hao kushindwa kusimamia maagizo na maelekezo yaliyotolewa tangu mwaka juzi kuhusu ukusanyaji wa kodi ya ardhi, uingizaji wa wamiliki wa viwanja na mashamba kwenye mfumo wa malipo kwa njia ya kielekroniki wa ardhi na utoaji wa hati za madai kwa wadaiwa sugu wa kodi ya ardhi. Mabula alisema pamoja na barua iliyoandikwa na Kamishna wa Ardhi Msaidiz...
Fahamu yote yaliyojiri katika Magazeti ya Tanzania leo ALHAMISI january 17, 2019. Hapa unapata habari zote zilizopewa uzito katika kurasa za mbele na kurasa za nyuma za habari za michezo na burudani.
Comments