MWILI
wa mtu mmoja ambaye jina lake halijajulikana umekutwa ukiwa umefungwa
kwenye kiroba na kutupwa kando ya barabara katika eneo la Karibu na Chuo
cha Ustawi wa Jamii mkabala na Ofisi za Kituo cha Sheria na Haki za
Binadamu (LHRC), kilichopo Kijitonyama jijini Dar es Salaam.
Mtu
huyo ambaye hakufahamika hata jinsia yake kutokana na namna ambavyo
kiroba hicho kilikuwa kimefungwa juu na chini, anadaiwa huenda aliawa na
mwili wake kutupwa ndani ya mfereji katika eneo hilo.
Global TV Online imefunga safari
mpaka eneo la tukio na hii ndiyo hali halisi ilivyokuwa baada ya kuukuta
mwili huo huku wananchi wa eneo hilo wakihamaki kutokana na tukio hilo
la kinyama.
Na ANDREW MSECHU-DAR ES SALAA KITUO kikubwa cha biashara cha kimataifa kinatarajiwa kujengwa katika eneo la Stendi ya Mabasi ya Ubungo, ujenzi utakaoanza Januari mwakani na kuchukua miezi 18 kukamilika. Akizungumza na MTANZANIA jana, Meneja wa Mauzo wa Kampuni ya East Africa Commercial & Logistics Center Tom Zhang, alisema kitakapokamilika kituo hicho kinatarajiwa kuwa namba moja kwa nchi za Afrika Mashariki. Alisema kwa sasa tayari wana vituo viwili vya aina hiyo, cha kwanza kikiitwa Dragon Mall ambacho kipo nchini Dubai na kingine kikiitwa Yiwu City Mall nchini China. “Kituo hiki kitakuwa maalumu kwa ajili ya kuingiza bidhaa kutoka nje na kuuza bidhaa kwenda nje. Kutakuwa karibu na kila kitu kinachohitajika kwa ajili ya biashara za kimataifa. “Hii ina maana kwamba kikishakamilika, hakutakuwa na sababu ya mfanyabiashara wa Tanzania kusafiri kwenda China au nje ya nchi kununua bidhaa na kuzileta nchini. Safari hizo zinagharimu muda mwingi na gharama kub...
Comments