MWILI
wa mtu mmoja ambaye jina lake halijajulikana umekutwa ukiwa umefungwa
kwenye kiroba na kutupwa kando ya barabara katika eneo la Karibu na Chuo
cha Ustawi wa Jamii mkabala na Ofisi za Kituo cha Sheria na Haki za
Binadamu (LHRC), kilichopo Kijitonyama jijini Dar es Salaam.
Mtu
huyo ambaye hakufahamika hata jinsia yake kutokana na namna ambavyo
kiroba hicho kilikuwa kimefungwa juu na chini, anadaiwa huenda aliawa na
mwili wake kutupwa ndani ya mfereji katika eneo hilo.
Global TV Online imefunga safari
mpaka eneo la tukio na hii ndiyo hali halisi ilivyokuwa baada ya kuukuta
mwili huo huku wananchi wa eneo hilo wakihamaki kutokana na tukio hilo
la kinyama.
Zitto ni mchawi, kaniroga sana kashindwa na sio raia wa Tanzania- Katibu UVCCM Kigoma Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Kigoma, Agustino Matefu amepokea zaidi ya wanachama 100 kutoka chama cha ACT-Wazalendo. Katika mkutano huo wa kuwapokea wanachama hao uliofanyika jijini Dar es salaam, wanachama hao wakiwemo madiwani wamesema kuwa, wameamua kukihama chama hicho baada ya kuona kinakosa muelekeo. “Kama mnavyoona waandishi wa habari, hawa wote siwajui lakini wameamua kuniita ili waweze kujiunga na chama cha mapinduzi CCM, na hizi ni salamu kwa Zitto kwamba 2020 atafute kazi ya kufanya au arudi kwao Kongo,”amesema Matefu.
Comments