MWILI
wa mtu mmoja ambaye jina lake halijajulikana umekutwa ukiwa umefungwa
kwenye kiroba na kutupwa kando ya barabara katika eneo la Karibu na Chuo
cha Ustawi wa Jamii mkabala na Ofisi za Kituo cha Sheria na Haki za
Binadamu (LHRC), kilichopo Kijitonyama jijini Dar es Salaam.
Mtu
huyo ambaye hakufahamika hata jinsia yake kutokana na namna ambavyo
kiroba hicho kilikuwa kimefungwa juu na chini, anadaiwa huenda aliawa na
mwili wake kutupwa ndani ya mfereji katika eneo hilo.
Global TV Online imefunga safari
mpaka eneo la tukio na hii ndiyo hali halisi ilivyokuwa baada ya kuukuta
mwili huo huku wananchi wa eneo hilo wakihamaki kutokana na tukio hilo
la kinyama.
Staa wa Bongo Fleva, Omary Nyembo. MUNGU mkubwa! Ndivyo unavyoweza kusema baada ya staa wa Bongo Fleva, Omary Nyembo kutolewa katika hospitali ya University Hospital of Dusseldorf ya nchini Ujerumani alikokuwa amelazwa baada ya kupata nafuu na kupelekwa Mombasa nchini Kenya. Akizungumza na Risasi Jumamosi, baba mzazi wa staa huyo, Faraji Nyembo alisema anamshukuru Mungu na Watanzania kwa maombi yao kwani mwanaye huyo kwa sasa ana nafuu na amepelekwa Kenya kwa ajili ya kuhudhuria kliniki. Aliendelea kueleza kuwa kwa sasa afya ya Dimpoz imeendelea kuimarika ambapo amefanikiwa kuruhusiwa kutoka hospitali ikiwa ni baada ya kufanyiwa oparesheni kubwa ya koo na sasa yupo nchini Kenya anakofanya kliniki pamoja na kupumzika pia. “Mwanangu sasa anaendelea vizuri kwani upasuaji aliofanyiwa umempa nafuu na hivi ninavyoongea na wewe ameruhusiwa kutoka hospitali nchini Ujerumani na yupo Kenya anakofanyia kliniki yake akisimamiwa na meya wa Mombasa ambaye ndiye anayempatia m...
Ijumaa , 21st Dec , 2018 Na Mwandishi wetu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Maguful, amebainisha sababu za kufanya mabadiliko kwenye Jeshi la Magereza kuwa ni kutokana kutoa fedha ambazo aliagiza kujengwa kwa nyumba za maaskari lakini mpaka sasa hazijajengwa. Rais Magufuli Rais Magufuli ametoa kauli hiyo Jijini Dar es salaam wakati akizungumza kwenye hafla ya utoaji vyeo kwa wahitimu wa maofisa na Ukaguzi, ambapo ameshangazwa kutoa mabilioni ya fedha kwa ajili ya askari magereza lakini hakuna iliyojengwa. " Kule Magereza nilitoa pesa kwa ajili ya kujenga nyumba za askari magereza pale Ukonga, zile nyumba mpaka leo hazipo na hela zimeisha, ndiyo maana nilifanya mabadiliko haraka haraka pale ". " Niwaeleze ukweli huwa ninauvumilivu lakini uvumilivu wa kwenye fedha huwa unanishinda, unatoa nyumba kwa ajili ya maaskari lakini hakuna kinachojengwa, nimemuagiza Kamishna Magereza azifuatilie h...
MWANDISHI WETU – Dar es Salaam WAKATI keshokutwa Wakristo wote duniani wataadhimisha Sikukuu ya Krismasi na wiki ijayo Mwaka Mpya wa 2019, vigogo 29 watasherehekea wakiwa mahabusu katika magereza mbalimbali nchini. Vigogo hao ni wale wanaoshtakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam wakituhumiwa kwa kesi mbalimbali, zikiwamo za uhujumu uchumi, biashara ya dawa za kulevya na meno ya tembo. Miongoni mwa vigogo hao ni Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko. Mbowe na Matiko watasherehekea Krismasi na Mwaka Mpya gerezani baada ya kufutiwa dhamana zao katika kesi ya uchochezi inayowakabili pamoja na wengine saba wa chama hicho. Kesi hiyo inatarajiwa kuendelea Januari 3, mwakani ikiwajumuisha washtakiwa wengine; Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa, Mbunge wa Kibamba, John Mnyika, Katibu wa Chadema, Dk. Vincent Mashinji, Mbunge wa Bunda, Esther Bulaya na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Zanzibar), Sa...
Comments