MWILI
wa mtu mmoja ambaye jina lake halijajulikana umekutwa ukiwa umefungwa
kwenye kiroba na kutupwa kando ya barabara katika eneo la Karibu na Chuo
cha Ustawi wa Jamii mkabala na Ofisi za Kituo cha Sheria na Haki za
Binadamu (LHRC), kilichopo Kijitonyama jijini Dar es Salaam.
Mtu
huyo ambaye hakufahamika hata jinsia yake kutokana na namna ambavyo
kiroba hicho kilikuwa kimefungwa juu na chini, anadaiwa huenda aliawa na
mwili wake kutupwa ndani ya mfereji katika eneo hilo.
Global TV Online imefunga safari
mpaka eneo la tukio na hii ndiyo hali halisi ilivyokuwa baada ya kuukuta
mwili huo huku wananchi wa eneo hilo wakihamaki kutokana na tukio hilo
la kinyama.
Comments