MWANDISHI WETU – Dar es Salaam WAKATI keshokutwa Wakristo wote duniani wataadhimisha Sikukuu ya Krismasi na wiki ijayo Mwaka Mpya wa 2019, vigogo 29 watasherehekea wakiwa mahabusu katika magereza mbalimbali nchini. Vigogo hao ni wale wanaoshtakiwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam wakituhumiwa kwa kesi mbalimbali, zikiwamo za uhujumu uchumi, biashara ya dawa za kulevya na meno ya tembo. Miongoni mwa vigogo hao ni Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe na Mbunge wa Tarime Mjini, Esther Matiko. Mbowe na Matiko watasherehekea Krismasi na Mwaka Mpya gerezani baada ya kufutiwa dhamana zao katika kesi ya uchochezi inayowakabili pamoja na wengine saba wa chama hicho. Kesi hiyo inatarajiwa kuendelea Januari 3, mwakani ikiwajumuisha washtakiwa wengine; Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa, Mbunge wa Kibamba, John Mnyika, Katibu wa Chadema, Dk. Vincent Mashinji, Mbunge wa Bunda, Esther Bulaya na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema (Zanzibar), Sa...
Comments