Viongozi wa upinzani wafanya kikao cha siri Zanzibar


Viongozi wa vyama vya siasa vya upinzani nchini wamejichimbia visiwani Zanzibar kwa ajili ya kupatiana mafunzo mbalimbali juu ya mwenendo wa siasa na demokrasia.
Viongozi waliohudhuria ni Katibu Mkuu wa Chama Cha Wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamadi, pamoja na Mjumbe wa Kamati Kuu ya CHADEMA, Edward Lowassa na Kiongozi wa ACT – Wazalendo Zitto Kabwe.
Mbali na hao, viongozi wengine walionekana na Rais wa Chama Cha Mawakili Tanzania, (TLS) Fatma Karume pamoja viongozi wengine mashuhuri nchini ambapo imeelezwa walijadili juu ya mwenendo wa hali ya kisiasa nchini.
Aidha, Kaimu Msemaji wa chama cha CUF, Mbarara Maharagande amesema kuwa kikao hicho kimeandaliwa na taasisi ya Marekani IR kupitia kwa Katibu wa CUF, Maalim Seif.
“Ni kweli kuna semina inafanyika ya viongozi wa vyama inafanyika Zanzibar ambayo inafanyika kwa siku tatu, na aliyewaalika ni Katibu Mkuu wetu Maalim Seif na imeandaliwa na taasisi ya IRSA, watu wa democratic ya America,” amesema Maharagande.

Comments

Popular posts from this blog

KESI YA ZITTO MUSWADA WA SHERIA YA VYAMA VYA SIASA YAHAMISHWA

Waziri asimamisha likizo za Marubani ATCL