Lukuvi, Makonda Wacharukia Migogoro ya Ardhi Gongo la Mboto


Lukuvi ameanza ziara yake leo
katika Wilaya ya Ilala akiambatana na viongozi wa Mkoa akiwemo Mkuu wa
Mkoa wa Dar es Salaam Paul Makonda, Mkuu wa Wilaya ya Ilala Sophia Mjema
na Maafisa Ardhi wa Wilaya ili kuweza kutatua kero zinazohusiana na masuala ya Ardhi na migogoro ya nyumba.
Akiwa katika ziara yake hiyo kwenye viwanja vya
Kampala vilivyopo Gongo la Mboto, Makonda amemwelezea Waziri Lukuvi
jinsi ambavyo amekuwa akijitahidi kusikiliza kero za wananchi kuhusiana
na migogoro ya Ardhi na kuwapatia elimu ya namna ya kumiliki Ardhi kwa
kufuata sheria na kuwa na hati miliki ya eneo husika.



https://youtu.be/G_aoaD7JqgI to see video
Comments