Posts

AJIUA , AMWACHIA MWANAYE BAISKELI !

Image
B UKOBA:  Salvatory Rweyemamu (47) ni baba aliyekuwa mkazi wa Kashai Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera ambaye anadaiwa kujiua kwa kujinyonga kwa kile kilichodaiwa ni hali ngumu ya maisha na kusumbuliwa na ugonjwa kisha kumwachia mwanaye baiskeli kama urithi.   Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, Rweyemamu aligundulika kuwa amefariki dunia kwenye chumba chake alichokuwa akiishi katika nyumba ya mwanamke aliyetajwa kwa jina la Tausi Ally. Ilielezwa kuwa, mwili wa Rweyemamu uligundulika Januari 6, mwaka huu, majira ya saa 3:00 asubuhi baada ya mtoto wa kaka yake kwenda kumjulia hali. Habari kutoka eneo hilo la tukio zilidai kwamba, mara baada ya kijana huyo kufika nyumbani kwa marehemu Rweyemamu alibisha hodi kwa muda mrefu bila kujibiwa. Ilielezwa kuwa, baada ya kuona hali hiyo, kijana huyo ilibidi aulizie kwa majirani ndipo majirani hao na rafiki wa marehemu, Andrew John walipochungulia kwa dirishani na kugundua mwili wa Rweyemamu ulikuw

LEO IJUMAA NDEGE MPYA YA SERIKALI KUTUA TANZANIA

Image
Airbus A220-300 iliyopewa jina la Ngorongoro. Ndege nyingine mpya ya Serikali aina ya Airbus A220-300 iliyopewa jina la Ngorongoro inatarajia kuwasilini nchini kesho Ijumaa mchana, ambapo itafanya idadi ya ndege zilizonunuliwa na Serikali kufikia sita. Ndege hiyo ambayo tayari inanakshi za Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) endapo itakodishwa kwa shirika hilo kama ilivyofanyika kwa ndege nyingine tano itafanya jumla ya ndege za ATCL kufikia 7, ikijumlishwa na ndege yao ya zamani aina ya Bombardier Q300 ambayo sasa ipo katika matengenezo. Ndege inayotarajiwa kutua kesho ni ya pili ya aina hiyo, kwani Desemba 23 iliwasili ya kwanza ambayo ilipewa jina la Dodoma. Ndege nyingine zinazomilikiwa na shirika hilo ni Bomberdier Q400-8 tatu na Boeing 87-8 (Dreamliner) moja. Tangu Serikali ya awamu ya tano iingie madarakani Novemba 5, 2015 imekuwa ikipigania kulifufua shirika hilo ambalo ilikuta likitawala soko la ndani kwa asilimia mbili likiwa na ndege moja aina Bombardier Q30

AJIUA , AMWACHIA MWANAYE BAISKELI !

Image
B UKOBA:  Salvatory Rweyemamu (47) ni baba aliyekuwa mkazi wa Kashai Manispaa ya Bukoba mkoani Kagera ambaye anadaiwa kujiua kwa kujinyonga kwa kile kilichodaiwa ni hali ngumu ya maisha na kusumbuliwa na ugonjwa kisha kumwachia mwanaye baiskeli kama urithi.   Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo, Rweyemamu aligundulika kuwa amefariki dunia kwenye chumba chake alichokuwa akiishi katika nyumba ya mwanamke aliyetajwa kwa jina la Tausi Ally. Ilielezwa kuwa, mwili wa Rweyemamu uligundulika Januari 6, mwaka huu, majira ya saa 3:00 asubuhi baada ya mtoto wa kaka yake kwenda kumjulia hali. Habari kutoka eneo hilo la tukio zilidai kwamba, mara baada ya kijana huyo kufika nyumbani kwa marehemu Rweyemamu alibisha hodi kwa muda mrefu bila kujibiwa. Ilielezwa kuwa, baada ya kuona hali hiyo, kijana huyo ilibidi aulizie kwa majirani ndipo majirani hao na rafiki wa marehemu, Andrew John walipochungulia kwa dirishani na kugundua mwili wa Rweyemamu ulikuwa ukininginia kwenye dari. Ilid

BREAKING: Upinzani yanyakua kiti cha urais kongo

Image
  Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo imemtangaza Mgombea wa Chama kikuu cha Upinzani Felix Tshisekedi kuwa mshindi wa nafasi ya Urais kwa asilimia 38.57 ya kura zote. Martin Fayulu ameshika nafasi ya pili huku Emmanuel Ramazani Shadary wa Chama tawala akiwa ameshika nafasi ya tatu. Hii ni mara ya kwanza Upinzani kushinda nchini Congo tangu nchi hiyo ilipopata Uhuru wake. Mkuu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Ceni) Corneille Nangaa, alisema mapema Alhamisi kwamba Bw Tshisekedi alipata asilimia 38.57 ya kura zilizopigwa na "anatangazwa mshindi wa urais mteule." Tshisekedi alipata zaidi ya kura 7 milioni naye bw Fayulu akapata kura takriban 6.4 milioni, huku mgombea wa serikali Emmanuel Ramazani Shadary akipata takriban kura 4.4 milioni. Rais Joseph Kabila anatarajiwa kuondoka madarakani baada ya kuongoza kwa miaka 18. Mgombea wake aliyemteua kuwakilisha muungano tawala Emmanuel Ramazani Shadary amemaliza wa tatu.

MPYA:! YALIYOJILI LEO 10/01/2019

Image