MAMLAKA ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) imetaja sababu nane za kufuta safari za ndege za Shirika la Fastjet Tanzania na kuipa notisi ya siku 28 kujieleza kwanini wasifutiwe leseni ya kuendesha biashara hiyo nchini. Wakati TCAA ikieleza hayo, Waziri wa zamani wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Lawrence Masha, ambaye ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika hilo na mwanahisa mkubwa wa Fastjet Tanzania, alipotafutwa kuzungumzia hali hiyo alisema yupo kwenye kikao. Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Hamza Johari, alitaja sababu hizo kuwa ni kutokuwa na ndege baada ya moja kati ya mbili zilizosajiliwa nchini kuharibika na kupelekwa nje ya nchi kwa matengenezo, huku moja ikizuiwa na mamlaka hiyo. Ndege hiyo ilizuiwa baada ya kampuni iliyowakodishia Fastjet kuitaka irudishwe kwa kile walichodai kuwa inafanya kazi bila wao kupata chochote. Alisema kutokana na uamuzi huo wa mkodishaji kutaka arejeshewe ndege yake, alilazimika kuizuia kama am...
Comments