KESI YA ZITTO MUSWADA WA SHERIA YA VYAMA VYA SIASA YAHAMISHWA

KESI ya Kiongozi wa ACT Wazalendo na wenzake wa vyama 10 vya upinzani ya kupinga muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa iliyopangwa kusikilizwa na jopo la majaji watatu wa Mahakama Kuu leo majira ya saa 3 asubuhi, limehamishiwa kwa Jaji mmoja.

Shauri la kesi hiyo lilipangwa kusikilizwa na Majaji; Barke Sehel (kiongozi wa jopo), Benhajo Masoud na Salma Maghimbi, lakini limekwama baada ya wajibu maombi (Serikali) kuwasilisha pingamizi la awali wakiitaka Mahakama hiyo ilitupilie mbali.

Aidha, kutokana na pingamizi hilo, Mahakama imesitisha usikilizwaji wa shauri la msingi na badala yake imeamua kuanza kusikiliza pingamizi ambapo imepanga kusikiliza pingamizi hilo na jaji Masoud katika chemba kuanzia saa 4:00, asubuhi.

Zitto na Viongozi wa Upinzani kwenye Kesi Yao Mahakama Kuu Leo

Comments

Popular posts from this blog

Waziri asimamisha likizo za Marubani ATCL