MAJAMBAZI:! Alhaj Mzee Yusuph na Mkewe wavamiwa

Aliyekuwa Msanii wa Taarabu nchini Alhaj Mzee Yusuph amevamiwa na Majambazi Usiku wa kuamkia Leo akiwa nyumbani kwake na familia yake.

Kwa mujibu wa Mzee Yusuph ameeleza kuwa akiwa nyumbani kwake Chanika usiku huu na familia yake ghafla walivamiwa na majambazi watatu na walivyoingia mzee anasema alipiga makelele sana kuomba msaada kwa majirani lakini hakupata msaada.

Pia amesema badala yake ikabidi apambane nao mwenyewe akitumia mawe na panga na kwasababu wavamizi hao hawakuwa na silaha za moto bali walitumia baruti kuwatisha watu wasisogee eneo la tukio hata hivyo walikimbia Ila walifanikiwa kuchukua simu na vitu vingine vidogovidogo, na Mke wake Leyla Rashidi amepata majeraha kidogo na hivyo amekimbizwa hospitali kwa ajili ya kupata matibabu

Comments

Popular posts from this blog

KESI YA ZITTO MUSWADA WA SHERIA YA VYAMA VYA SIASA YAHAMISHWA

Waziri asimamisha likizo za Marubani ATCL