Hatimaye mili ya watu 11 kati ya 15 waliofariki katika ajali
iliyohusisha Magari mawili ya abiria na kusababisha vifo katika kijiji
cha komaswa wilayani Tarime Mkoani Mara na kushindwa kutambuliwa,
imetambuliwa kupitia vinasaba huku mili mingine minne ikishindwa
kutambuliwa kabisa.
Ajali hiyo ilitokea Novemba 26,2018 baada ya magari hayo kugogana uso
kwa uso kisha kuwaka moto na kusababisha watu kuungua na mili yao
kushindwa kutambulika hatua iliyopeleka serikali kuamua kuzika eneo la
pamoja,na kufanya uchunguzi wa vinasaba ili kuweza kuwatambua.
Akitoa taarifa hiyo mkoani humo mkuu wa Mkoa wa mara Adamu Malima
amesema baada ya miili hiyo 11 kutambuliwa serikali ya mkoa imepanga
kwenda kuweka vibao vyenye majina ya marehemu Decenba 23 sambamba na
ujenzi wa mnara.
Malima amesema kuwa serikali haitamzuia ndugu wa marehemu ambao watataka
kuchukua mili ya wapendwa wao baada ya kutambuliwa kwaajili mazishi kwa
taraibu za kimila na kidini kulingana na imani zao ambapo amesema
watatakiwa taratibu za ufukuaji wa mili ikiwemo kuapata kibali cha
mahakama.pia
Katika ajali hiyo jumla ya watu 17 walifariki Dunia ambapo 15 walifariki
papo hapo na wengine watatu wakiokolewa ambapo mmoja alifariki akiwa
njiani kupelekwa hospital na mmoja alifariki hospital ya Rufaa ya
Bugando jijini Mwanza akipatiwa matibabu.
Serikali ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), imekemea ushawishi unaotolewa na kanisa Katoliki unaodai kuwa wanajua kiongozi aliyeshinda katika uchaguzi wa rais. Barnabe Kikaya Bin Karubi ambaye ni msemaji wa 'Common front for the Congo', ameiambia BBC kuwa "Jambo linalofanywa na kanisa ni kitu ambacho hakikubaliki, ni sawa na kuwaandaa watu kufanya mapinduzi". Serikali ya mseto imesisitiza kwamba ni Tume ya uchaguzi peke yake ndio inaweza kutangaza matokeo ya uchaguzi. Matokeo ya uchaguzi wa urais DRC 'kuchelewa' Huduma ya intaneti yafungwa DR Congo siku moja baada ya uchaguzi Wagombea wa upinzani walalamikia dosari uchaguzi DRC Kanisa Katoliki, ambalo lina ushawishi mkubwa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, limesema kuwa kuna mshindi wazi wa urais katika uchaguzi uliofanyika Jumapili, kwa mujibu wa matokeo ambao wamefanikiwa kuyaona. Maaskofu wa kanisa hilo wamewataka watawala nchini humo kuwa wakweli na kutangaza matokeo hayo karib...
NAIBU Waziri wa Ardhi, Nyumba na Makazi, Dk. Angelina Mabula amewavua nyadhifa wakuu wa Idara ya Ardhi katika Manispaa ya Kigoma Ujiji na Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kwa kushindwa kutekeleza majukumu yao ya kazi ipasavyo. Waliovuliwa nyadhifa hizo ni Mkuu wa Idara ya Ardhi wa Manispaa ya Kigoma, Brown Nziku, Mkuu wa Idara ya Ardhi Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma, Emanuel Magembe na Ofisa Ardhi Mteule, Paul Misuzi. Mabula alifanya uamuzi huo Januari 3, mwaka huu akiwa mkoani hapa baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika Manispaa ya Kigoma Ujiji na Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma. Alifikia uamuzi huo baada ya watendaji hao kushindwa kusimamia maagizo na maelekezo yaliyotolewa tangu mwaka juzi kuhusu ukusanyaji wa kodi ya ardhi, uingizaji wa wamiliki wa viwanja na mashamba kwenye mfumo wa malipo kwa njia ya kielekroniki wa ardhi na utoaji wa hati za madai kwa wadaiwa sugu wa kodi ya ardhi. Mabula alisema pamoja na barua iliyoandikwa na Kamishna wa Ardhi Msaidiz...
Fahamu yote yaliyojiri katika Magazeti ya Tanzania leo ALHAMISI january 17, 2019. Hapa unapata habari zote zilizopewa uzito katika kurasa za mbele na kurasa za nyuma za habari za michezo na burudani.
Comments