Hatimaye mili ya watu 11 kati ya 15 waliofariki katika ajali
iliyohusisha Magari mawili ya abiria na kusababisha vifo katika kijiji
cha komaswa wilayani Tarime Mkoani Mara na kushindwa kutambuliwa,
imetambuliwa kupitia vinasaba huku mili mingine minne ikishindwa
kutambuliwa kabisa.
Ajali hiyo ilitokea Novemba 26,2018 baada ya magari hayo kugogana uso
kwa uso kisha kuwaka moto na kusababisha watu kuungua na mili yao
kushindwa kutambulika hatua iliyopeleka serikali kuamua kuzika eneo la
pamoja,na kufanya uchunguzi wa vinasaba ili kuweza kuwatambua.
Akitoa taarifa hiyo mkoani humo mkuu wa Mkoa wa mara Adamu Malima
amesema baada ya miili hiyo 11 kutambuliwa serikali ya mkoa imepanga
kwenda kuweka vibao vyenye majina ya marehemu Decenba 23 sambamba na
ujenzi wa mnara.
Malima amesema kuwa serikali haitamzuia ndugu wa marehemu ambao watataka
kuchukua mili ya wapendwa wao baada ya kutambuliwa kwaajili mazishi kwa
taraibu za kimila na kidini kulingana na imani zao ambapo amesema
watatakiwa taratibu za ufukuaji wa mili ikiwemo kuapata kibali cha
mahakama.pia
Katika ajali hiyo jumla ya watu 17 walifariki Dunia ambapo 15 walifariki
papo hapo na wengine watatu wakiokolewa ambapo mmoja alifariki akiwa
njiani kupelekwa hospital na mmoja alifariki hospital ya Rufaa ya
Bugando jijini Mwanza akipatiwa matibabu.
Na ANDREW MSECHU-DAR ES SALAA KITUO kikubwa cha biashara cha kimataifa kinatarajiwa kujengwa katika eneo la Stendi ya Mabasi ya Ubungo, ujenzi utakaoanza Januari mwakani na kuchukua miezi 18 kukamilika. Akizungumza na MTANZANIA jana, Meneja wa Mauzo wa Kampuni ya East Africa Commercial & Logistics Center Tom Zhang, alisema kitakapokamilika kituo hicho kinatarajiwa kuwa namba moja kwa nchi za Afrika Mashariki. Alisema kwa sasa tayari wana vituo viwili vya aina hiyo, cha kwanza kikiitwa Dragon Mall ambacho kipo nchini Dubai na kingine kikiitwa Yiwu City Mall nchini China. “Kituo hiki kitakuwa maalumu kwa ajili ya kuingiza bidhaa kutoka nje na kuuza bidhaa kwenda nje. Kutakuwa karibu na kila kitu kinachohitajika kwa ajili ya biashara za kimataifa. “Hii ina maana kwamba kikishakamilika, hakutakuwa na sababu ya mfanyabiashara wa Tanzania kusafiri kwenda China au nje ya nchi kununua bidhaa na kuzileta nchini. Safari hizo zinagharimu muda mwingi na gharama kub...
Comments