Hatimaye mili ya watu 11 kati ya 15 waliofariki katika ajali
iliyohusisha Magari mawili ya abiria na kusababisha vifo katika kijiji
cha komaswa wilayani Tarime Mkoani Mara na kushindwa kutambuliwa,
imetambuliwa kupitia vinasaba huku mili mingine minne ikishindwa
kutambuliwa kabisa.
Ajali hiyo ilitokea Novemba 26,2018 baada ya magari hayo kugogana uso
kwa uso kisha kuwaka moto na kusababisha watu kuungua na mili yao
kushindwa kutambulika hatua iliyopeleka serikali kuamua kuzika eneo la
pamoja,na kufanya uchunguzi wa vinasaba ili kuweza kuwatambua.
Akitoa taarifa hiyo mkoani humo mkuu wa Mkoa wa mara Adamu Malima
amesema baada ya miili hiyo 11 kutambuliwa serikali ya mkoa imepanga
kwenda kuweka vibao vyenye majina ya marehemu Decenba 23 sambamba na
ujenzi wa mnara.
Malima amesema kuwa serikali haitamzuia ndugu wa marehemu ambao watataka
kuchukua mili ya wapendwa wao baada ya kutambuliwa kwaajili mazishi kwa
taraibu za kimila na kidini kulingana na imani zao ambapo amesema
watatakiwa taratibu za ufukuaji wa mili ikiwemo kuapata kibali cha
mahakama.pia
Katika ajali hiyo jumla ya watu 17 walifariki Dunia ambapo 15 walifariki
papo hapo na wengine watatu wakiokolewa ambapo mmoja alifariki akiwa
njiani kupelekwa hospital na mmoja alifariki hospital ya Rufaa ya
Bugando jijini Mwanza akipatiwa matibabu.
Comments