Ofisa habari wa Simba, Haji Manara jana alitokwa na machozi ya furaha
baada ya kufanikiwa kupindua meza kibabe kwenye mchezo wa Ligi ya
Mabingwa dhidi ya Nkana FC ya Zambia na kuwashukuru mashabiki kujitokeza
kuipa sapoti.
Simba walifanikiwa kushinda kwa mabao 3-1 uwanja wa nyumbani na
kufanikiwa kushinda kwa jumla ya mabao 4-3 baada ya matokeo ya awali
Simba kukubali kichapo cha mabao 2-1.
Manara amesema kuwa walijipanga na waliwaambia mashabiki wao wajitokeze
kwa wingi uwanja wa Taifa ili kuwapa morali wachezaji kupambana na
ndivyo ilivyotokea.
"Ujinga huwa unakuwa wakati wa kwenda tu wakati wa kurudi hakuna kitu
kama hicho, tunawashukuru mashabiki kwa kujitokeza kwa wingi na sapoti
yao waliyotoa hatimaye yametia," alisema.
Zitto ni mchawi, kaniroga sana kashindwa na sio raia wa Tanzania- Katibu UVCCM Kigoma Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Kigoma, Agustino Matefu amepokea zaidi ya wanachama 100 kutoka chama cha ACT-Wazalendo. Katika mkutano huo wa kuwapokea wanachama hao uliofanyika jijini Dar es salaam, wanachama hao wakiwemo madiwani wamesema kuwa, wameamua kukihama chama hicho baada ya kuona kinakosa muelekeo. “Kama mnavyoona waandishi wa habari, hawa wote siwajui lakini wameamua kuniita ili waweze kujiunga na chama cha mapinduzi CCM, na hizi ni salamu kwa Zitto kwamba 2020 atafute kazi ya kufanya au arudi kwao Kongo,”amesema Matefu.
Comments