Bunge lavunjwa kuitisha uchaguzi mpya 2019

Viongozi wa vyama vinavyounda Serikali ya Mseto ya Israel wamekubaliana kulivunja Bunge na kuitisha uchaguzi  mpya Aprili 2019.
Baada ya mkutano wa leo Jumanne kwa sauti moja wamekubaliana kuvunja Bunge na kuitisha uchaguzi mapema baada ya muhula wa miaka minne.
Hatua hiyo imefikiwa huku kukiwa na mvutano ndani ya Serikali ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu ya siasa za mlengo wa kulia.
Netanyahu amekabiliwa na shinikizo la madai ya ufisadi, huku waendesha mashtaka wakimtafutia sababu za kumfungulia mashtaka tokea mwanzoni wa mwaka.
Hata hivyo, ripoti zinasema kuwa Mkuu wa zamani wa Jeshi la Ulinzi la Israeli (IDF), Benny Gantz, anajiandaa kugombea kama mgombea binafsi hali ambayo inaweza kusababisha ugumu wa kutabiri matokeo.
Netanyahu ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama cha Likuda amehudumu kama Waziri Mkuu wa Israel tangu 2009 mpaka sasa.

Comments

Popular posts from this blog

KESI YA ZITTO MUSWADA WA SHERIA YA VYAMA VYA SIASA YAHAMISHWA

Waziri asimamisha likizo za Marubani ATCL