Waziri awaonya madaktari nchini


Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amewaonya madaktari kote nchini kuacha tabia za kuwa madalali wa Maduka ya dawa kwa kuwaandikia wagonjwa dawa mara mbili mbili.

Waziri Ummy ameagiza hospitali za Rufaa kote nchini kuhakikisha zinakuwa na maduka ya dawa litakalokuwa  na uhakika wa dawa zote muhimu ili kuondosha kero hiyo na kuondoa mianya ya madaktari kudalalia dawa kwenye maduka binafsi.

Hata hivyo amesema kuwa watakaobainika watachukuliwa hatua kali za kisheria.

Comments

Popular posts from this blog

KESI YA ZITTO MUSWADA WA SHERIA YA VYAMA VYA SIASA YAHAMISHWA

Waziri asimamisha likizo za Marubani ATCL