WADAU WOTE WA ELIMU MNATANGAZIWA KUWA ,NOTES ZA MASOMO YA SAYANSI KWA VITENDO (PRRACTICAL) BIOLOGY ,PHYSICS, CHEMISTRY KWA UPANDE WA OLEVEL, ZINAPATIKANA HAPA ZINGINE PIA
KESI ya Kiongozi wa ACT Wazalendo na wenzake wa vyama 10 vya upinzani ya kupinga muswada wa Sheria ya Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa iliyopangwa kusikilizwa na jopo la majaji watatu wa Mahakama Kuu leo majira ya saa 3 asubuhi, limehamishiwa kwa Jaji mmoja. Shauri la kesi hiyo lilipangwa kusikilizwa na Majaji; Barke Sehel (kiongozi wa jopo), Benhajo Masoud na Salma Maghimbi, lakini limekwama baada ya wajibu maombi (Serikali) kuwasilisha pingamizi la awali wakiitaka Mahakama hiyo ilitupilie mbali. Aidha, kutokana na pingamizi hilo, Mahakama imesitisha usikilizwaji wa shauri la msingi na badala yake imeamua kuanza kusikiliza pingamizi ambapo imepanga kusikiliza pingamizi hilo na jaji Masoud katika chemba kuanzia saa 4:00, asubuhi. Zitto na Viongozi wa Upinzani kwenye Kesi Yao Mahakama Kuu Leo
WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isaak Kamwelwe, amesimamisha likizo za marubani wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL) katika kipindi cha mwisho wa mwaka. Amesema marubani wa ATCL ambao wameshaanza likizo wanapaswa kurudi kazini na kuendelea na kazi ya kutoa huduma kwa wananchi. Kamwelwe aliyasema hayo jana muda mfupi baada ya kuwasili Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) akitokea mkoani Mbeya kwenye ukaguzi wa Uwanja wa Kimataifa wa Ndege wa Songwe (SIA). Alisema wafanyakazi wa Mamalaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) nao hawapaswi kwenda likizo kipindi hiki cha mwisho wa mwaka bali wanapaswa kuhakikisha magari yaendayo mikoani hayapandishi nauli. "Hakuna Mtanzania atakayepata shida ya kusafiri kipindi hiki cha sikukuu. Tumejipanga kusafirisha abiria hadi usiku," alisema Waziri Kamwelwe. Alisema maofisa wa Sumatra wanapaswa kuhakikisha abiria hawaonewi wala kusumbuliwa na wenye mabasi hususani eneo l
Comments