Mke aongea Mumewe Sheikh kutekwa kwa siku ya tisa leo


Leo December 14, 2018 Taarifa kutoka Shule ya Sekondari Islamiya iliyopo Nyakato Mwanza zinasema Mwalimu Mkuu kitengo cha Dini Sheikh Bashiru Habibu ametekwa kwa siku ya tisa leo na Watu wasiofahamika.
AyoTV na millardayo.com imezungumza na Mke wa Sheikh na kusimulia namna alivyopokea taarifa ya mume wake kutekwa kwa siku ya tisa leo.
“Sisi tulipata taarifa siku ya tukio jioni na mpaka leo sijui Mume wangu alipo, ila alichukuliwa na gari akiwa eneo la Shule na lilikuwa halina namba” Mke wa Sheikh


 


Comments

Popular posts from this blog

KESI YA ZITTO MUSWADA WA SHERIA YA VYAMA VYA SIASA YAHAMISHWA

Waziri asimamisha likizo za Marubani ATCL