Haswa :CCM yazidi kujiimarisha
Mwandishi Wetu, Dar es Salaam Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimemrejeshea uanachama wa chama hicho aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dares Salaam, Ramadhani Madabida na wenyeviti wengine wanne baada ya kujiridhisha na maombi yao ya kutaka kusamehewa kwa makosa yao wakiwa wenyeviti wa chama hicho. Aidha, halmashauri hiyo, imemuweka chini ya uangalizi aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Iringa, Jesca Msambatavangu, ambaye pia ameomba kurejeshewa uanachama baada ya kufukuzwa kwa makosa ya kimaadili. Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Jumanne Desemba 18, Katibu Mkuu wa CCM, Dk. Bashiru Ally, amewataja waliosamehewa pamoja na Madabida ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Mkoa wa Shinyanga, Erasto Kwirasa, Christopher Sanya (Mara) na aliyekuwa Mwenyekiti wa chama hicho Wilaya ya Kinondoni, Salum Madenge. “Hatua hiyo imefikiwa leo katika kikao cha halmashauri ya chama kilichoongozwa na Mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli ambapo pamoja na mamb...
Comments